https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, April 08, 2015

Zakhem FCna FFU SC kusaka Bingwa wa jumla michuano ya Ligi ya Mkoa Dar es Salaam

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
Baada ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na kupata timu tatu zitakazouwakilisha mkoa katika michuano ya ligi ya mabingwa ya mikoa ya TFF,kesho Alhamis Aprili 09/2015,katika uwanja wa Karume jijini kutakuwa na mchezo wa fainali ya kumpata Bingwa wa jumla wa michuano ya ligi ya mkoa.
Msemaji wa DRFA Omary Katanga, pichani
Msemaji wa Chama cha Soka Mkoa Dar es Salaam (DRFA), Omary Katanga, alisema kwamba timu zitakazoumana katika fainali hiyo ni ZAKHEM FC dhidi ya FFU SC,ambazo zitashuka dimbani majira ya saa kumi jioni zikishuhudiwa na umati wa mashabiki waliokuwa wakiyafuatilia mashindano hayo tangu yalipoanza kutimua vumbi.

Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha soka mkoa wa Dar es salaam DRFA,timu zilizofanikiwa kuuwakilisha mkoa katika michuano ya ligi ya maabingwa ni pamoja na ZAKHEM FC,FFU SC na CHANGANYIKENI SC.

Mwenyekiti wa DRFA, Almas Kasongo,ameipongeza kamati hiyo ya mashindano kwa kusimamia vizuri uendeshaji wa ligi tangu ilipoanza.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...