https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, April 01, 2015

Barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam yafungwa rasmi

Sasa barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam inafungwa rasmi kuanzia leo Jumatano ya  01/04/2015. Kikao Maalum kilichowahusisha Wadau mbalimbali Kutoka kwenye Taasisi za Serikali kimekamilika punde na kukubaliana kufunga Rasmi Barabara ya Msimbazi ifikapo saa sita usiku leo. Wadau waliohusika kama inavyoonekana pichani ni pamoja na; 1. DART 2. Manispaa ya Kinondoni 3. Manispaa ya Ilala 4. 

Halmashauri ya Jiji 5. SUMATRA 6. TANROADS 7. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa 8. SMEC 9. STRABAG 10. JESHI LA POLISI. Mabadiliko mbalimbali ni pamoja na kubadilika kwa mielekeo mbalimbali ya Magari kutoruhusiwa kutumia barabara ya Msimbazi. Fuata maelekezo ya viashiria mbalimbali ili kukuepushia usumbufu. 

TUNAJENGA KWA AJILI YAKO TUNAOMBA USHIRIKIANO WAKO. Tunaomba Taarifa hii uitume kwenye Makundi mengine au kwa Rafiki yako ili kusaidia kusambaa kwa Taarifa hii muhimu kwa Wakazi wa Jiji la Dar es salaam. 
 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...