https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, April 02, 2015

King Majuto ‘kuvunja mbavu’ Zanzibar siku ya KARUME DAY, Aprili 7

Na Andrew Chale
Msanii mkali wa maigizo na vichekesho, Nchini, Amri Athuman a.k.a King Majuto anatarajiwa kufanya shoo maalum ya vichekesho katika viwanja vya kufurahia watoto Kariakoo, Aprili 7, mwaka huu Mjini Unguja, Zanzibar.

Kwa mujibu wa wandaaji wa shoo hiyo kampuni ya Bond Entertainment Limited, kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), walieleza kuwa gwiji huyo wa vichekesho King Majuto ambaye pia ni mkongwe anayetamba ndani na nje ya Tanzania ataonyesha vichekesho vyake hivyo hiyo Aprili 7, katika mapumziko ya siku ya Karume (KARUME DAY).
mzee
KingMajuto“Ni wakati wa familia kujitokeza kwa wingi siku ya Jumanne ya tarehe 7/4/2015, kuja kumshuhudia King Majuto na kufurahia vichekesho vyake” ilieleza taarifa hiyo.
Ambaapo katika siku hiyo ya Aprili 7, kwenye shoo hiyo ya vichekesho, kiingilio kwa wakubwa ni Tsh.2,000/= huku kwa watoto itakuwa ni sh 1,000.

wema_2Pichani ni baadhi ya vichekesho vyaa gwiji huyo, King Majuto katika moja ya kazi zake akiwa na msanii Wema Sepetu.

Onyesho hilo lenye vionjo vya “Njoo uvunje mbavu na King Majuto!!. Taarisha mbavu zako” limedhaminiwa na kampuni ya mawasiliano ya tigo Tanzania.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...