https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, April 04, 2015

Jamal Malinzi akutana na Makamu wa Rais wa FIFA

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF jana ijumaa ilipokea ugeni wa makamu wa Rais wa FIFA ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu nchini Jordan, HRH Prince Ali Bin Al Hussein pichani.

Jioni Prince Ali Bin AliHussein na ujumbe wake walifanya mazungumzo na Rais wa Shrikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF Jamal Malinzi  katika hoteli ya Kilimanjaro Kempsinki (Hyatt) iliyopo jijini Dar es salaam.

Katika mazungumzo hayo, zaidi waligusia maeneo kadhaa ya ushirikiano kati ya TFF na Chama cha Mpirwa wa Miguu nchini Jordan (JFA), hasa katika maeneo ya maendeleo ya mpira wa vijana, makocha na waamuzi.

HRH Prince Ali Bin Al Hussein ambaye ni mgombea wa nafasi ya urais FIFA mwaka huu, ameondoka leo mchana kurudi nyumbani kwake Jordan.
  

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...