https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, April 06, 2015

Dayna Nyange kuachia wimbo mpya uitwao 'Nitulize', akiimba na Nay wa Mitego

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MWMBAJI wa kike wa muziki wa kizazi kipya Mwanaisha Said ‘Dayna’ Jumatano anaachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Nitulize’, akiimba kwa ushirikano mkubwa na Nay wa Mitego.
Dayna na Nay wa Mitego wanavyoonekana katika kava ya wimbo mpya uitwao Nitulize ulioimbwa na Dayna akimshirikisha Nay wa Mitego.

Wimbo huo unatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake kwa wadau na mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva unaozidi kutesa katika sehemu mbalimbali za Tanzania na nje ya nchi kwa ujumla. Akizungumza na Mtandao wa Handeni Kwetu, Dayna alisema kuwa wimbo huo mpya umetengenezwa na mtayarishaji wake T Touch kutoka Studio za Free National Sound.

Alisema wimbo huo utakuwa moto wa kuotea mbali kutokana na aina ya uimbaji uliochanganya sauti mbili za Dayna na Nay wa Mitego, moja ya wasanii wanaofanya makubwa katika tasnia hiyo. “Huu ni wimbo wa aina yake kutokana na jinsi nilivyotulia katika uimbaji wangu na nilivyoweza kutuliza akili yangu, huku nikifurahishwa zaidi na Nay wa Mitego alivyoweza kuimba.

“Naomba mashabiki wangu wakae mkao wa kula baada ya kuachia kibao change hiki keshokutwa Jumatano katika vituo mbalimbali vya radio, ukiwa ni mwendelezo wa kuonyesha makali yangu,” alisema.
Dayna aliwahi kutesa na nyimbo kadhaa ikiwamo ile ya Mafungu ya Nyanya, Nivute Kwako, Fimbo ya Mapenzi, ambazo kwa pamoja ziliweza kumtangaza vyema katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...