https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, April 13, 2015

Bundi wa ajari barabarani aiandama Tanzania,18 wafariki Iringa na Burudani chupuchupu kuua 50 Lushoto


Basi linaloitwa Nganga Express likiteketea kwa moto mkoani Morogoro jana
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
WIMBI la ajali nchini Tanzania linaendelea kutikisa, baada ya mkoani Morogoro watu 18 kudaiwa kufariki papo hapo jana asubuhi baada ya basi linaloitwa Nganga Express yenye namba za usajili T.373 BAH kugongana uso kwa uso na Mitsubish Fuso T.164 BKG maeneo ya Milima ya Udzunwa kando ya Mto Ruaha na basi hilo kuwaka moto, mkoani Morogoro.
Watu wa karibu waliokuwa kwenye ajali hiyo walisema kwamba watu 15 walifariki kutoka kwenye basin a wengine 3 kufariki kutoka kwenye fuso, ambapo majeruhi ni 10, huku wanaume wakiwa 6 na wanawake 4.
Majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya St Kizito Mikumi na wengine wakilazwa katika Hospitali ya Mtandika, mkoani Iringa. Katika ajali hiyo, pia inadaiwa kuwa pikipiki moja iliteketea kwa moto na kuongeza kuwa inahisiwa pikipiki hiyo ndiyo chanzo cha kuripuka kwa moto huo. 

Wakati huo huo jana jioni iliripotiwa kuwa basi linalojulikana kama Burudani nusura liangamize roho za watu 50 baada ya kutaka kutumbukia mtaroni Soni, wilayani Lushoto


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...