https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, April 09, 2015

Mwendokasi watajwa chanzo cha ajali iliyoua 10 na kujeruhi 35 Handeni, Tanga

Na Mwandishi Wetu,Tanga
AJALI iliyoangamiza roho za watu 10 katika kijiji cha Mbweni Mkata, wilayani Handeni, mkoani Tanga, umetajwa kuwa chanzo cha ajali hiyo iliyohusisha gari ya Ratco na Ngorika zilizogongana baada ya gari ndogo aina ya Passo nayo kugongana na Ratco.
 Hali ilivyoonekana katika ajali ya magari matatu ambayo ni Ratco, Ngorika na gari ndogo ya Passo
Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani mkoani Tanga, Abdi Issango, aliuambia mtandao wa Handeni Kwetu kuwa mwendo kasi ndio uliosababisha ajali hiyo na kusababisha vifo vya watu 10, wakiwamo madereva wawili na abiria wao nane.

Ajali hiyo ilitokea leo saa tano asubuhi ambapo awali Ratco iligongana na Passo ambapo pia ikajumlisha na basi la Ngorika lililokuwa linatoka Dar es Salaam kuelekea Arusha.

Majeruhi 35 katika ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya wilaya Korogwe (Magunga), Handeni na ile ya Mkata kwa ajili ya kuwapatia matibabu majeruhi hao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...