https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, June 15, 2014

Uchaguzi Mkuu Simba wasimamishwa hadi kuundwa kwa Kamati ya Maadili Simba



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
SHIRIKISHO la Mpira wa miguu Tanzania (TFF), limeusimamisha Uchaguzi Mkuu wa klabu ya Simba, hadi hapo watakapofanikiwa kuunda kwa Kamati ya Maadili itakayokuwa na jukumu la kusikiliza malalamiko yote yanayohusiana na wagombea wao.

Kusimamishwa huko kumekuja siku chache baada ya mchakato wa uchaguzi wa Simba kuanza, ambapo Kamati ya Uchaguzi ya Simba, chini ya Damas Ndumbaro ilimuengua Michael Wambura kuwania Urais wa klabu hiyo, kabla ya Kamati ya Rufaa kumrudisha kwa madai kuwa uovu upo kwa Simba, si Wambura.

Akizungumzia hilo leo mchana, jijini Dar es Salaam, Rais wa Shirikisho hilo, Jamal Malinzi, alisema kuwa Simba inapaswa kuunda Kamati ya Maadili kabla ya Juni 30 ili kusikiliza mashauri yatakayoletwa mbele yake na kuyatolea ufafanuzi, jambo ambalo huenda likapokewa kwa shingo upande wa wadau wa soka Tanzania, maana klabu hiyo imetumia gharama hususan wale waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...