https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, June 12, 2014

Qs Mhonda: Mb Dog ndio mpinzani wa Diamond


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MKURUGENZI wa Qs Mhonda J Entertainment, Joseph Mhonda, amesema kwamba mwenye uwezo wa kupunguza makali ya mwimbaji Nassib Abdul Diamond ni Mbwana Mohamed ‘Mb Dog’ pekee.
Msanii Diamond, pichani.
Akizungumzia hilo, jijini Dar es Salaam, Mhonda alisema hiyo inatokana na ubora wa wasanii hao, pamoja na aina yao inayovitia kuwasikiliza.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Qs Mhonda J Entertainment, Joseph Mhonda pichani.
Alisema Diamond ni msanii mkali ambaye kwa mtindo wake huenda akakosa mpinzani, kama Mb Dog atazidi kushuka thamani yake kisanaa.
Msanii Mb Dog, pichani.
“Kila nikimuangalia Diamond Napata shauku ya kuona makali ya Mb Dog yanarudi kwasababu ndio anayeweza kuleta ushindani kwa mwimbaji huyo anayetamba na mtindo wake wa Ngololo.

“Mb Dog ana ladha nzuri, sambamba na uimbaji wake unaovutia bila kusahau ubunifu pia katika tungo zake, hivyo kwa kiasi kikubwa yeye ndio mpinzani wa kweli wa Diamond na si mwingine,” alisema.

Mb Dog kwa sasa anatamba na wimbo wake Mbona Umenuna, akiimba kwa hisia kubwa, huku akiwa na shauku ya kurudi makali yake ya zamani.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...