https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, June 13, 2014

Binslum aijaza mapesa Stand United ya Shinyanga



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MFANYABIASHARA kutoka Kampuni ya BinSlum Tires, Nassor BinSlum, ameingia mkataba wa kudhamini klabu ya Stand United yenye maskani yake Shinyanga wa mwaka mmoja.
Nassor BinSlum akikabidhi jezi itakayotumiwa na timu ya Stand United ya Shinyanga katika Ligi ya Tanzania Bara msimu ujao wa Ligi baada ya kupanda daraja, huku kampuni yake ikiwadhamini kwa mwaka mmoja.

Stand United watavuna kiasi cha Sh Milioni 50 kwa mwaka, huku wakiahidiwa kuongezwa fedha nyingine pindi watakapoonyesha kiwango kizuri msimu huu.


Akizungumzia leo mchana wakati wa kuingia mkataba na klabu hiyo, mbele ya mlezi wao Steven Masele, ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga Mjini,
BinSlum pichani.
BinSlum alisema lengo lake ni kuisaidia klabu hiyo ili ifikie malengo yake.

Alisema ingawa fedha hizo zinaonekana kama kidogo, lakini timu hiyo ikionyesha soka la kuvutia, basi watavuna udhamini mwingine mnono hata kwa wafanyabiashara weengine.

“Tunataka kuona kuwa timu zetu kwa pamoja zinapiga hatua kubwa kupata wadhamini wengine, hivyo kampuni yangu itahakikisha kuwa inafanya juhudi kukuza soka la Tanzania.

"Stand United ifanye bidii kubwa kuonyesha kuwa wanaweza kucheza soka, nikiamini kuwa hali hiyo itakuwa na manufaa makubwa kwa soka la Tanzania,” alisema.

Naye mlezi wa klabu hiyo, Masele alimshukuru BinSlum kwa uamuzi wake mzuri wa kuidhamini klabu yao, wakiamini kuwa mwendo huo utakuwa na manufaa makubwa kwa upande wao.

Katika hatua nyingine, Masele aliwaambia waandishi wa habari kuwa amejitolea kuwanunulia basi dogo la kusafiria timu hiyo iliyozaliwa Stendi mjini Shinyanga.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...