https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, June 04, 2014

George Tyson aagwa Leaders Club tayari kwa safari ya Kenya kwa maziko Juni 14 mwaka huu

Mzazi mwenzake marehemu, Monalisa, akilia kwa uchungu wakati anaaga jeneza la George Otieno Tyson, Leaders Club leo mchana. Mwili wake utasafirishwa kesho na utazikwa Juni 14 nchini Kenya, baada ya kufariki kwa ajali ya gari Ijumaa iliyopita mkoani Dodoma.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWILI wa marehemu George Otieno ‘Tyson’, umeagwa leo kuanzia asubuhi hadi saa tisa alasiri katika viwanja vya Leaders Club, huku ukitarajiwa kusafirishwa kesho asubuhi kuelekea nchini Kenya.



Mara baada ya kufika Kenya, Tyson atazikwa katika makaburi ya Siaya, Kisumu nchini Kenya Juni 14 mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiq, akiaga mwili wa marehemu, George Otieno Tyson, Leaders Club leo mchana.
Maandalizi ya kumuaga Tyson leo Leaders Club.....
Wasanii wakitoa jeneza la marehemu George Otieno Tyson baada ya kumaliza kuaga. Mwili wake utasafirishwa kesho na utazikwa Juni 14 nchini Kenya, baada ya kufariki kwa ajali ya gari Ijumaa iliyopita mkoani Dodoma.

Mzazi mwenzake marehemu, Monalisa, akilia kwa uchungu.
Mmiliki wa Blog hii, Kambi Mbwana, wa pili, akishiriki kumuaga muongozaji wa filamu George Otieno Tyson, Leaders Club leo mchana. Mwili wake utasafirishwa kesho na utazikwa Juni 14 nchini Kenya, baada ya kufariki kwa ajali ya gari Ijumaa iliyopita mkoani Dodoma.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...