https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 24, 2012

Watoto wa Mukajanga waanzisha kampuni ya mitindo



 Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WATOTO wa Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubu Mukajanga, wameanzisha kampuni yao ya mitindo, inayojulikana kama TRIDASHANZ Business  Modeling kwa ajili ya kuendeleza vipaji vyao vya mitindo.

        Watoto wa Kajubi Mukajanga, Patricia na dada yake Sanza katikati 

Watoto hao ni Sanza Mukajanga na ndugu yake Patricia, ambao kwa vipindi tofauti walishiriki mashindano ya urembo, likiwamo Miss Dar City Centre kwa Patricia na Sanza, aliyeshiriki shindano la Miss Chang’ombe na wote kuingia katika nafasi nzuri katika patashika hizo za urembo.

Akizungumza jana na HANDENI KWETU jijini Dar es Salaam, Sanza, alisema kwamba wameamua kuanzisha kampuni hiyo kwa ajili ya kufanya kazi mbalimbali zinazohusu sanaa, ikiwamo ya kuandaa shoo za mitindo, urembo na mengineyo.

    Katibu wa Baraza la Habari (MCT), Kajubi Mukajanga 
Alisema ujio wa kampuni hiyo ni mwelekeo mpya wa kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya sanaa hapa nchini, wakiamini kuwa malengo yao waliyojiwekea yatatatimia kwa kuwa karibu na mitindo.

“Ni harakati za kimaendeleo zaidi  huku nikiamini kuwa tufanikisha mipango yetu ya kuibua pua vipaji vipya vya mitindo au urembo, ukizingatia kwa miaka kadhaa tumefanya sanaa ya aina hiyo.

“Kwa sasa tunachofanya ni kuweka mikakati ya kushirikisha wanamitindo mbalimbali katika programu zetu tulizoweka kabla ya kuanzisha kampuni hii ambayo kwa kiasi Fulani itakuwa na mafanikio makubwa,” alisema Sanza.

Kwa mujibu wa Sanza, tayari warembo zaidi ya 10 wameanza mazoezi ya mitindo katika Ukumbi wa Golden Bridge, uliopo maeneo ya Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam mapema wiki hii.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...