https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 17, 2012

Kagera nayo yaivuta Simba mkia



                                          Amri Kiemba akijituma uwanjani leo
                                          
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MABINGWA watetezi, Simba SC, leo wameendelea kuvutwa mkia baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na timu ya Kagera Sugar, mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Simba yalipatikana dakika ya 8 likifungwa na Felix Sunzu na 53 liliofungwa na Mrisho Ngassa, wakati mabao ya Kagera Sugar yalifungwa na Temi Felix dakika ya 63 kwa shuti kali na Salum Kanoni aliyeifungia timu yake kwa njia ya penati, dakika ya 66.

Licha ya kutoka sare hiyo, Simba bado wanaendelea kuongoza ligi hiyo yenye ushindani wa aina yake na kila timu ikipania kushinda katika mechi zake.

Mpira ulianza kwa kasi ya ajabu, huku Kagera wakionekana kupagawa zaidi, ingawa nafasi kadhaa ilizopata ilishindwa kuzitumia.

Mwamuzi wa mchezo huo alikuwa ni Reonald Swai kutoka jijini Arusha aliyechezesha pambano hilo lililokuwa na upinzani wa aina yake.

Wachezaji walioanza katika mechi hiyo dhidi ya Simba ni pamoja na Andrew Ntalla, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Amandus Nesta, Benjamin Affe, Maleges Mwanga, Daud Jumanne, George Kavilla, Shija Mkina, Enyinna Darlington na Wilfred Ammeh.

Wakati Simba walioanza ni Juma Kaseja, Said Chollo, Amir Maftah, Juma Nyoso, Paschal Ochieng, Mwinyi Kazimoto, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba, Felix Sunzu, Haruna Moshi 'Boban' na Emmanuel Okwi.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...