https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, October 19, 2012

Ngwasuma kesho jumamosi hapatoshi Makumbusho


     Nyosh Al Sadaat
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WAZEE wa Ngwasuma, FM Academia, kesho Jumamosi wanafanya shoo ya aina yake katika Ukumbi wa Kijiji Cha Makumbusho, uliopo Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, huku wakipania kuwapa burudani za aina yake mashabiki wao.

Onyesho hilo linafanyika huku bendi hiyo ikitamba na nyimbo mbalimbali, ukiwamo ule wa Otilia, wimbo unaopendwa vilivyo na mashabiki wao katika kumbi wanazokuwapo wakali hao wa dansi nchini.

Akizugumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Kelvin Mkinga, alisema kwamba mashabiki wao waende kwa wingi kujionea manjonjo yao katika tasnia hiyo nchini.

Alisema wanamuziki wao wamekuwa wakifanya shoo za aina yake, wakiwa na lengo la kuonyesha makali yao, hivyo mashabiki wao waendelee kupokea burudani safi kutoka kwa vijana wao.

“FM Academia ni bendi kongwe na imara sana katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini, hivyo naamini mashabiki wetu wataendelea kutuunga mkono kwa ajili ya kuwapatia burudani zaidi.

“Naamini sisi ni wakali na hatuna mpinzani, hivyo jukumu letu ni kufanya kazi nzuri zaidi kwa kutunga nyimbo na kuandaa shoo za aina yake, ukizingatia tuna watu mahiri kuanzia waimbaji hadi wanenguaji,” alisema Mkinga.

FM Academia ipo chini ya Rais wa Vijana, Nyosh Al Sadaat, sambamba na wakali wengine, akiwamo Patchou Mwamba, ambaye pia ni mkali katika tasnia ya filamu hapa nchini, akishiriki katika filamu mbalimbali.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...