https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, October 19, 2012

Twanga na Facebook Mzalendo Pub Jumapili


    Kalala Junior akiwaimbisha mashabiki wa Twanga Pepeta
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya muziki wa dansi hapa nchini ya The African Stars, Twanga Pepeta, jumapili inatarajia kufanya shoo ya aina yake, waliyoipa jina la Facebook Fans, itakayofanyika katika Ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama.

Kufanyika kwa shoo hiyo ni kuwaweka sawa na kuwakumbuka mashabiki wao wanaoendelea kuwaunga mkono kwa miaka 11 sasa walipoanzisha bendi hiyo inayopendwa na watu wengi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa ASET, Hassan Rehani, alisema mashabiki wao wote, wakiwamo waandishi wa habari na wadau wengine watakumbukwa na kuthaminiwa mchango wao.

Alisema kwamba bendi yao imekuwa ikipita katika vipindi mbalimbali, hivyo wanaamini mafanikio yao kwa sasa yamesababishwa na watu wengi, jambo linalowafanya waandae part hiyo hiyo usiku wa facebook na Twanga.

“Tumekuwa tukifanya vizuri katika soko la muziki wa dansi kutokana na mchango wa kila mmoja wetu, hivyo naamini wadau wote tutakutana katika Ukumbi huo wa Mzalendo na kucheza pamoja kisigino.

“Twanga ni bendi ya kila mmoja, hivyo nadhani changamoto zinazoonekana kwa sasa ni sehemu ya kutufanya tuwe juu zaidi, huku tukiamini kada mbalimbali na jinsi tofauti tutakutana ili tucheze pamoja,” alisema.

Twanga Pepeta ipo chini ya Luiza Mbutu pamoja na waimbaji mbalimbali wenye uwezo wa juu, akiwamo Kalala Junior aliyejiunga na bendi yake hiyo, akitokea Mapacha Watatu na maswahiba zake, Jose Mara na Khalid Chokoraa, huku Ally Akida, Chokoraa, Soud Mohammed au MCD na wengineo wakithibitisha kushiriki katika onyesho hilo kutokana na kuwahi kufanya kazi na bendi hiyo kwa nyakati tofauti.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...