https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 17, 2012

Wachezaji sita wafariki ajalini Kagera


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za vifo vya wachezaji watano wa timu ya Rusumo FC ya mkoani Kagera vilivyotokea jana jioni (Oktoba 16 mwaka huu).
 
                                         Angetile Osiah, Katibu Mkuu wa TFF                                          
 Rusumo FC ilikuwa ikitoka kwenye mechi ya michuano ya Polisi Jamii Wilaya ya Ngara ambapo ikiwa njiani kurudi Rusumo kutoka mjini Ngara ilipata ajali ya gari na wachezaji watano kufariki papo hapo.

Wachezaji wengine ambao ni majeruhi wamelazwa Hospitali ya Wilaya ya Ngara ya Murugwanza huku wawili hali zao zikiwa mbaya.

Msiba huo ni pigo kwa familia za marehemu, klabu ya Rusumo FC, Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Ngara (NDFA), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA) na familia ya mpira wa miguu kwa ujumla nchini kutokana na mchango wa wachezaji hao katika ustawi wa mchezo huu kupitia klabu yao.

TFF inatoa pole kwa familia za marehemu, Rusumo FC, NDFA na KRFA na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Kutokana na msiba huo, mechi zote za Ligi Kuu ya Vodacom zinazochezwa leo (Oktoba 17 mwaka huu) kutakuwa na dakika moja ya maombolezo ili kutoa heshima kwa marehemu hao. Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...