https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, October 23, 2012

ALBERT SANGA





                                       Aliyepania kuwakomboa Watanzania

                                         Albert Sanga, Mkurugenzi wa Fresh Farm T (Ltd)

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KUNA juhudi kubwa zinazofanywa na baadhi ya Watanzania, hasa kwa kuanzisha makampuni ya aina mbalimbali kwa ajili ya kuwakomboa wenzao.

Makampuni hayo yanajishughulisha kwa biashara mbalimbali, hivyo kuwa njia nzuri ya kuwapatia maisha bora kama wataendeleza mikakati hiyo.



Miongoni mwa watu hao ni Albert Sanga, mjasiriamali aliyeanzisha Kampuni ya utunzaji wa mazingira ya Fresh Farm (T), yenye makazi yake wilayani Mufindi, mkoani Iringa.

Kusudio kubwa ni kuokoa mazingira na kuwatajirisha watanzania kwa kuwekeza kwenye kilimo cha miti ambayo ni biashara nzuri kwa miaka ya leo na kesho, hivyo kujikomboa zaidi katika maisha yao endapo watajiingiza humo.

“Lazima nikiri kilimo cha miti kimepata umaarufu kwa miaka ya karibuni kutokana na ongezeko la mahitaji ya mazao ya miti na changamoto ya mazingira, huku Iringa tukiongoza kwa misitu mikubwa ya kupandwa.


“Sasa hii miti inatumika kwa mbao, nguzo za umeme, nguzo za kujengea pamoja na utengenezeaji wa karatasi na kuyaachia mashirika ya kimazingira kutoka Ulaya wakati ardhi ni ya kwetu na utajiri huo unakwenda kwao,” alisema.

Kwa kupanda shamba la miti na kukusanya dola kwa kuuza hewa ukaa wakati ukisubiri miti ikomae na kuvuna mbao, nguzo ama miti ghafi ya kutengenezea karatasi, ni uokoaji wa mazingira kwa kiasi kikubwa.

Anasema alianzisha biashara hiyo kwa miaka minne iliyopita na kujiwekea malengo ya kupanda miti ekari ishirini kila mwaka, huku kilimo hiki cha miti kikiwa ni uwekezaji wa muda wa kati na mrefu, ingawa Watanzania wengi hawavutiwi na uwekezaji wa muda mrefu.

Sanga ambaye ni mtaalamu wa biashara anasema kwamba namna bora ya kunufaika kiuchumi, ni uwekezaji wa muda mrefu, Waingereza wanasema ‘Information is power’, hivyo Ulaya na Amerika wananunua hewa ya Ukaa na kutajirika zaidi kwa kupitia kilimo cha miti.

Anasema zipo ekari zinauzwa kwa utaratibu rasmi na kwa mujibu wa sheria ya ardhi ukizingatia kuwa ekari moja ya shamba inachukua wastani wa miti mia sita na wastani wa chini wa mti mmoja uliokomaa ni elfu 20,000.

“Ina maana katika ekari moja ukiwa na miti iliyokomaa unakusanya jumla ya shilingi milioni 12,000,000, ikiwa ni fedha za kadirio la chini ikiwa mkulima atauza bei ya jumla miti inapokuwa shambani.
 
“Lakini kama ukiamua kupasua mbao mwenyewe unaweza kuvuna mbao hadi za milioni ishirini na tano 25,000,000 kwa ekari moja huku kukiwa hakuna gharama za moja kwa moja hapa, ukizingatia kuwa Iringa ni mkoa wenye miundombinu nafuu,” alisema Sanga.

Sanga anasema kwamba gharama za kununua shamba tupu ni shilingi laki mbili hadi milioni moja na kutegemea na maeneo yanayotakiwa na mhusika, huku gharama za kuandaa shamba, kununua miche na kupanda ni kati ya shilingi 400,000 hadi laki 600,000.

Kilimo cha miti ni rahisi kwa sababu haihitaji uangalizi mkubwa muda wote na mvua inyeshe au isinyeshe, maana mti ya mbao, nguzo ama karatasi ukishachipua huwa haufi kwakuwa huendelea kutumia unyevu wa ardhini.

“Muhimu ni kutengeneza njia za kuzuia moto walau mara moja kwa mwaka, kazi ya pili ni kufyekea miti inapokua walau kwa mwaka mara moja (prooning) na kudai kuwa gharama hizi hazizidi laki laki mbili kwa mwaka.

“Kwa mfano ukichukua shilingi laki mbili kugharimia shamba kila mwaka ukazidisha mara sita unapata sh 1,200,000 na ukizidisha mara 10 unapata 2,000,000,” alisema.

Mkurugenzi huyo wa Fresh Farm (T) anasema mtu akiwa na shamba la miti leo; thamani ya ardhi hivyo kupata faida bila kuangalia umbali wa kuikuza miti hiyo kama wengi wao wanavyojidanganya kwamba biashara hii si ya muda mfupi.

Anasema mtu akishapanda shamba la miti la ekari moja na kuamua kuuza baada ya mwaka mmoja, basi mauzo yake hayatakuwa chini ya milioni mbili hadi nne.

Hivyo mtu huyo atakuwa amekusanya shilingi 4,000,000 kwa mtaji wa shilingi 600,000 bila kupata usumbufu wowote wa kusimamia.

Sanga anasema kwao msimu wa kutafuta na kuandaa mashamba ni Agosti na Oktoba, huku upandaji ukiwa ni Novemba, Desemba na Januari, ikiwa ni njia ya kuwasaidia wengine ili wawekeze katika biashara hii ya mashamba.
 
“Siku zote napenda kuendeleza wafanyabiashara na wawekezaji wapya kwa kupitia mfumo wa biashara zetu, hivyo tumeanzisha kitengo maalumu cha Fresh Farms (T) na kazi yetu kubwa itakuwa ni kupitia kitengo hiki itakuwa ni kutoa ushauri wa kibiashara, kutafuta maeneo ya kilimo cha miti hapa Iringa pamoja na kiasi heka anazotaka mteja,” alisema Sanga.

Kwa mujibu wa Sanga, Fresh Farm (T) inatumia sheria ya ardhi ya mwaka 1999, pia taratibu na tamaduni zote za wenyeji zinazohusiana na umilikaji ardhi, hivyo kuwa na uhakika wa kutunza mazingira na kuwatajirisha watanzania.

0712 053949
0753 806087

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...