https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, October 15, 2012

FM Academia kuvamia Hill Take Ijumaa


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya muziki wa dansi ya FM Academia, maarufu kama Wazee wa Ngwasuma, wanatarajia kufanya shoo ya nguvu katika Ukumbi wa Hill Take, uliopo Ukonga, jijini Dar es Salaam, Ijumaa ya Oktoba 19.

Kuvamia ukumbi huo ni sehemu ya kuwapatia burudani mashabiki wao wa Ukonga, wakiamini kuwa litaacha watu hoi kutokana na mipango yao waliyoiweka kwa ajili ya kufanya shoo ya nguvu na kuwaburudisha mashabiki wao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam na Handeni Kwetu, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa bendi hiyo, Kelvin Mkinga, alisema kwamba mipango kwa ajili ya shoo hiyo imekamilika kwa ajili ya kuwapatia raha mashabiki wao wa Ukonga.

Alisema bendi yao imekuwa ikitamba na nyimbo mbalimbali zinazopendwa na watu wengi, hivyo anaamini mashabiki wao watapata raha za aina yake na kuendelea kuwaunga mkono katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini.

“Ni bendi yenye mipango imara katika tasnia ya muziki wa dansi, hivyo naamini mashabiki wetu watakuja kwa wingi katika ukumbi huo kwa ajili ya kucheza na Wazee wa Ngwasuma wenye nyimbo zinazopendwa na wengi.

“Nyimbo kama ‘Heshima kwa Mwanamke’, ‘Otilia’ na nyinginezo ni kati ya zitakazoporomoshwa na waimbaji wetu, hivyo naaamini mashabiki watakuja kwa wingi kuburudika pamoja na kudhihirisha FM Academia ni zaidi yao,” alisema Mkinga.

FM Academia ipo chini ya Rais wa Vijana, Nyosh Al Sadaat, akiwa sambamba na wakali wengine akiwamo Patchou Mwamba, ambaye pia ni mkali katika tasnia ya filamu baada ya kushiriki katika filamu mbalimbali hapa nchini.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...