https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, October 18, 2012

Super D kumpika Ibrahim Mawe



                              Ibrahimu Mawe

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA Ibrahimu Mawe, maarufu kama 'King Class Mawe', anatarajia kuingia kambini mwishoni mwa wiki hii kujiandaa na kujiandaa na pambano lake na Said Mundi, anayetokea Tanga, kwa Wagosi wa Kaya, litakalopigwa Desemba 9, katika Ukumbi wa PTA, Sabasaba, jijini Dar es Salaam na kusubiriwa kwa hamu na mashabiki wa ngumi.

Maandalizi ya Class Mawe, yanakuja siku chache baada ya kushinda katika patashika yake na Jonas Segu wa Dar es salaam, aliyempiga na kuwafurahisha mashabiki wake katika mchezo huo wa masumbwi hapa nchini.

Akizungumza mapema leo mchana jijini Dar es Salaam, kocha wa mchezo wa masumbwi, Rajabu Mhamila, maarufu kama ‘Super D’, amesema bondia huyo atakuwa katika mikono yake kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo.

Alisema bondia wake ataanza mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na pambano hilo muhimu, akiwa na lengo la kufanya vizuri zaidi katika mchezo wa masumbwi na kurithi mikoba ya wapiganaji wengine waliotamba hapa nchini.

“Naomba wadau wampe sapoti kijana huyu katika pambano lake lijalo, ukizingatia kwamba nia ni kuhakikisha kuwa anapiga hatua zaidi katika mchezo wa masumbwi hapa nchini na kufikia malengo ya wakali wengine.

“Naamini kila kitu kitakuwa sawa, ndio maana Class ataingia kambini mapema kwa ajili ya kumnoa vizuri ili awe nyota na kutikisa katika ulingo wa masumbwi na kuupandisha chati kama wadau tunavyopania,” alisema.

Ibrahim Class ni miongoni mwa mabondia wanaochipukia kwa kasi hapa nchini, huku akiwa na mipango imara ya kuwachapa wapinzani wake katika mapambano mbalimbali yanayoandaliwa kwa ajili ya kuonyesha cheche zake.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...