https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, October 15, 2012

Milovan kuelezea sare yao na Coastal leo


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Milovan Cirkovic, leo anatarajia kuanika chanzo cha sare yake na Coastal Union ya Tanga pamoja na muendelezo wa ligi hiyo, huku wakikipiga na Kagera Sugar, kesho katika Uwanja wa Taifa.

Kutoka sale na Coasta Union kumepokelewa kwa shingo upande na mashabiki wa timu hiyo, hasa wale waliokwenda kuishuhudia mechi hiyo ya aina yake na kuipatia Simba pointi moja, hivyo kufikisha pointi 17.


                                         Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga

Simba wanaingia uwanjani kucheza na Kagera Sugar huku wakiwa na machungu ya kusimamishwa na Wagosi wa Kaya, licha ya kujipanga kwa ajili ya mchezo huo uliohudhuliwa na mashabiki wengi wa jijini Tanga na maeneo mengine ya nchi.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kocha huyo atazungumza yote yaliyosababisha asihndwe kupata pointi tatu kutoka kwa Wagosi wa Kaya, mechi iliyopigwa Jumamosi, katika Uwanja wa Mkwakwani.

Alisema kwamba anaamini kwa kujua mapungufu yake, ni sababu ya kuwaamisha mashabiki wake kuwa watashinda mbele ya Kagera Sugar wanaotoka mjini Bukoba na kuikuta Simba yenye machungu na mchezo huo.

“Simba tuna uchungu na mechi hiyo ya Kagera Sugar, ila sitaki kuzama sana kwenye mambo ya kiufundi maana yataongelewa na kocha wetu kwa ajili ya kuwatoa hofu mashabiki na wanachama wote hapa nchini.

“Naamini kuna mengi yametokea na yatatokea katika ligi hii yenye ushindani wa aina yake, lakini huenda limepatia ufumbuzi na kocha wetu, Milovan hivyo kuendeleza wimbi la ushindi na hatimae kunyakua ubingwa kwa mara ya pili mfululizo,” alisema Kamwaga.

Ligi ya Tanzania Bara imezidi kuwa na ushindani wa aina yake, huku kila timu ikipania kushinda katika mechi zake zote, jambo linalozifanya timu kongwe za Simba na Yanga zitumie nguvu kubwa ili kuzipa ushindi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...