https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 17, 2012

Usiku wa kizazi cha dansi ndani ya Extra Bongo

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo, kesho Ijumaa, wanatarajia kufanya shoo ya nguvu katika Ukumbi wao wa nyumbani wa White House, Kimara Korogwe, jijini Dar es Salaam.

Burudani hizo zitaongozwa na Mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki, sambamba na wakali wengineo wanaofanya vyema katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini.

                                           Ally Choki
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Choki alisema kwamba shoo yao hiyo itapambwa na wakali wao wote, akiwamo Rogert Hega 'Catapiler', Ramadhani Masanja ‘Banza Stone’ na Khadija Mnoga 'Kimobitel'.

Alisema kuwa usiku huo wa kizazi cha dansi utawahusisha wanamuziki hao walio na bendi hiyo katika maonyesho yatakayofanyika kweye kumbi Bongo Resort na Meeda Sinza.

Baadhi ya nyimbo zao ni 'Kila Chenye Mwanzo', 'Game 111', 'Nguzo Tano', 'Mtaji wa Maskini', 'Elimu ya Mjinga', 'Simba Ananguruma', 'Kumekucha', 'Mtu Pesa', 'Password',' Chuki Binafsi', 'Jirani', 'Umbeya hauna Posho', 'Fadhila kwa Wazazi' 'Mtenda Akitendewa', 'Mjini Mipango' na nyinginezo.

Aidha, onyesho hilo pia linatarajiwa kupambwa na kikundi cha burudani cha Baikoko na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Husein Machozi ambaye atakuwa anatambulisha wimbo wake mpya.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...