https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 24, 2012

Tino kuzindua filamu ya mapigano Ijumaa





Tino Muya

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKALI wa filamu hapa nchini, Tino Muya, kesho Ijumaa anatarajia kuizundua filamu yake mpya ya mapigano, inayojulikana kama (CID), katika Ukumbi wa Biashara Complex.

Filamu hiyo imeandaliwa kwa kiwango cha juu, huku ikiwa ya kwanza kwa msanii huyo kucheza filamu za mapigano, ukizingatia kwamba kwa muda mrefu amekuwa akicheza zile zinazoelezea uhusiano wa kimapenzi tu.

Akizungumza muda mfupi na HANDENI KWETU, Tino alisema kwamba filamu hiyo ipo kwenye ubora wa hali ya juu, huku akipanga kuizindua Ijumaa katika Ukumbi wa Biashara Complex, Kijitonyama.

Alisema wadau na mashabiki wa filamu watapata kutu kizuri kutoka kwake, akiandaa chini ya Kampuni yake ya Tino Muya Films Company, aliyoanzisha mwaka 2009 kwa ajili ya kujihusisha na sanaa hapa nchini.

“Ni matarajio yangu kuwa watu watapata kitu kizuri kutoka kwangu, huku nikiachana kabisa na filamu za mapenzi kwa ajili ya kubadilisha soko la filamu hapa nchini kutoka mapenzi hadi mapigano.

“Naamini wadau na mashabiki watakuja kwa wingi kujionea jinsi gani watu wanaingia katika ulimwengu mpya wa filamu, maana wasanii wengi na waandaaji wamekuwa wakitayarisha filamu za kimapenzi tu,” alisema Tino.

Filamu nyingine zilizoaandaliwa na kampuni hiyo ni pamoja na Hatia, Shoga Yangu, Nzowa, One Blood, Hazard, My Heart, Olopong, Means Day Out, End of the Day, Good Fellow, Rooleen na sasa CID, filamu ambayo imeandaliwa kwa ufanisi kwa nia ya kuleta mapinduzi kisanaa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...