https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 17, 2012

Chegge, Temba kupamba shindano la Mfalme wa Mic Dar Live


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
Shindano kabambe la kumsaka Mfalme wa Mic (The Mic King), litapambwa na wakali wa Bongo Fleva, Said Juma ‘Chegge’ na Amani James Temba ‘Mheshimiwa Temba’.

                                                       Said Juma, Chege
Kila kitu kuhusu shindano hilo ambalo mshindi wake atajinyakulia zawadi ya gari la kifahari ni Jumapili hii kwenye Ukumbi wa Dar Live, Mbagala Zakhem, Dar es Salaam.

Mratibu wa Shindano la The Mic King, Luqman Maloto amesema kuwa sambamba na Chegge pamoja na Temba, bi. Mkubwa anayetamba kwa sasa kwenye ulingo wa Bongo Fleva, Bi. Cheka, naye atakuwepo.

“Siku hiyo, kutakuwa na shoo maalum kwa wakali wapya kutoka timu ya Mkubwa na Wanawe kutambulishwa chini ya Meneja Said Fella ‘Mkubwa’,” alisema Luqman na kuongeza:

“Vilevile Bendi ya Extra Bongo ikiongozwa na Ally Choki, Banza Stone, Khadija Mnoga ‘Kibotel’ na Rogert Hegga ‘Katapila’, itakuwepo kufanikisha siku hiyo nzuri.”

Luqman aliongeza kuwa Jumapili iliyopita, walisakwa vijana 12 kutoka Temeke, wiki hii ni zamu ya Wilaya ya Ilala, nayo kushindana na kupata 12 Bora yao.

“Niwasihi tu mashabiki wajitokeze kwa wingi kwani msisimko tuliouona mwanzoni ulikuwa si wa kitoto. Ikumbukwe kwamba mshindi atajiondokea na gari la kifahari,” alisema Luqman.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...