https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, October 17, 2012

Tenisi ni mchezo matajiri?





                                          Mchezaji wa tenisi, Mohamed Dewji
Mchezo wa tenisi ni mzuri mno lakini wengi wanaoingia humo ni wale ambao wazazi wao wana chochote kitu. Sababu inayosababisha hilo ni namna ya mchezo wenyewe pamoja na vifaa vyake kuuzwa bei ghari mno.

Mtu ambaye hata kula yao nyumbani ni tabu, hawezi kutumia kiasi kikubwa cha pesa kununulia vifaa hivyo vya mchezo wa tenisi. Pichani ni mcheza tenisi, Mohamed Dewji, kama alivyokutwa na mpiga picha mahiri wa michezo, Rahel Pallangyo, leo katika Viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam.

Ipo sababu ya wadau kuliangalia suala hilo ili kuufanya mchezo huo ni wa watu wote badala ya wale wenye nazo, zikiwamo sura nyeupe kwa Tanzania. Wakati nasema hayo, soka ndio mchezo pekee kwa Tanzania ambao unavutia kuchezwa na kila mtu. 

Kwa maoni na ushauri
kambimbwana@yahoo.com
0712 053949
0753 806087

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...