https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, November 18, 2015

Twanga Pepeta yapata pigo, Mwinjuma Muumini ang'oa nyota wake watatu, akiwapo Dogo Rama, Salehe Kupaza na Jojoo Jumanne

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya Twanga Pepeta imepata pigo zito baada ya Mkurugenzi wa bendi ya Double M Sound, Mwinjuma Muumini kuwanyakua wanamuziki watatu ambao ni Dogo Rama, Salehe Kupaza na Jojoo Jumanne.
Mwanamuziki Dogo Rama enzi hizo wakati yupo bendi ya The African Stars, Twanga Pepeta, sasa amejiunga na bendi ya Double M Sound.
Kuondoka kwa wanamuziki hao ambao sasa wanaelekea nchini Msumbiji kuweka kambi ili kuimarisha bendi hiyo, kutaleta mshike mshike katika bendi hiyo inayomilikiwa na mjasiriamali Asha Baraka.

Mwanamuziki Dogo Rama aliyeibuliwa na Twanga Pepeta miaka kadhaa iliyopita aliuthibitishia mtandao huu kuwa ameamua kuhama rasmi katika bendi yake hiyo na kuhamia katika bendi ya Double M Sound.


Kuondoka kwa wanamuziki hao watatu katika kipindi  cha kuelekea mwishoni mwa mwaka kutapokewa kwa hisia tofauti na wadau wa muziki wa dansi nchini, ambapo Twanga imeendelea kubaki kileleni kwa kutegemea zaidi sauti na uwezo wa kutunga nyimbo wa Kupaza, aliyepika vibao moto moto.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...