https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, December 01, 2015

Ray Mboya ashinda umeya Manispaa ya Moshi kwa kofia ya Chadema


Msimamizi wa Uchaguzi wa nafasi ya Meya ndani ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Edward Makabayo akizungumza jambo wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo.
Baadhi ya Madiwani walioshiriki zoezi la kumpata Meya wa manispaa ya Moshi kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Meya wa Manispaa ya Moshi aliyemaliza muda wake na Mbunge wa sasa wa jimbo la Moshi mjini,Jafary Michael akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika Hotel ya Umoja.
Madiwani wakimsikiliza Mbunge Michael kwa makini .
Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro,Basil Lema akizungumza katika kikao hicho.
Waliokuwa washindani katika nafasi ya kuwania kuteuliwa na Chadema nafasi ya Meya wa manispaa ya Moshi,Francis Shio (kushoto)  akimpongeza Raymond Mboya baada ya kutangazwa mshindi kwa kupata kura 16 dhidi ya kura 10 za Shio .
Madiwani wakimpongeza Ray Mboya baada ya kutangazwa mshindi.
Raymond Mboya ambaye pia ni diwani wa kata ya Longuo akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi wa nafasi ya kuteuliwa na Chadema kupeperusha bendera katika nafasi ya kugombea kuwa Meya wa manispaa ya Moshi.
aliyekuwa akiogombea nafasi ya Meya ,Francis Shio akizungumza mara baada ya kushindwa na Ray Mboya huku akiwataka madiwani kuungana kufanya kazi ya ahadi walizotoa kwa wananchi.
Mshindi wa nafasi ya Naibu Meya ,Peter Minja akishukuru mbele ya madiwani waliompigia kura na kufanikiwa kushika nafasi hiyo.
aliyekuwa akigombea nafasi ya Naibu Meya ,Jomba Koi na kushindwa na Peter Minja akizungumza katika kikao hicho akitoa ahadi ya kushirikiana na Meya aliyechaguliwa.

Mwenyekiti wa baraza la wazee wa chadema manispaa yaMoshi,Ally Mwamba akizungumza jambo katika kikao hicho.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazin
i.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...