https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, February 16, 2015

Msanii TID amlilia baba yake Dully Sykes aliyefariki

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWIMBAJI wa Bongo Fleva, Khalid Mohamed maarufu kama (TID), pichani chini mwenye miwani, ameonyesha kuguswa na kifo cha baba wa msanii Dully Sykes, Abby Sykes, anatayetarajiwa kuzikwa leo mchana katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Msanii TID pichani...
Baba yake Dully Sykes, marehemu mzee Abby Sykes, pichani enzi za uhai wake.
Akizungumzia msiba huo, TID alisema kwamba marehemu alikuwa karibu naye, sambamba na kuwahi kuimba naye mara kadhaa.

“Mzee Abby Sykes alikuwa ni kama mzee wangu kwasababu nilikuwa karibu naye, hivyo nimepokea msiba huu kwa masikitiko makubwa,” alisema TID.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...