https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, February 02, 2015

Mwanaharakati wa maendeleo Misima, wilayani Handeni mkoani Tanga, Rashid Kilo auchambua udhaifu wa Mbunge Kigoda

HUU NI UTHIBITISHO TOSHA WA KUKUJUZA WEWE MWANA HANDENI KWAMBA MBUNGE WETU NI MBINAFSI NA MWENYE UCHU WA MADARAKA NA MWENYE KUJALI FAMILIA YAKE.
MH. Mbunge aliingia madarakani mnamo mwaka 1995, wakati Wilaya ya Handeni ikiwa ni moja na Kilindi. Baada ya kutawala miaka 5 aliomba ridhaa ya kuongoza tena mwaka 2000 lakini wakati huu tayari alishaanza kusikia manung'uniko toka kwa Wakilindi na Wanguu waliopo Kilindi sasa, kwa kuwa anawajuwa vizuri misimamo yao, alianza mchakato wa kuigawa Wilaya ili awatenge na kuendelea na wengine ambao kimsingi amewamudu.
Alifanikiwa lengo lake na mnamo 1-7-2002, Wilaya ya Handeni iligawanywa rasmi na ikapatikana Wilaya ya Kilindi. 


Rashid Kilo, mwanaharakati wa maendeleo wilayani Handeni, mkoani Tanga, pichani.
Mwaka 2005, aliomba ridhaa katika SHAMBA lake la Handeni na kupata, kudhihirisha kuwa ni mbinafsi alimpigania dada yake AISHA KIGODA nae akawa mbunge viti maalum toka Tanga. Lakini yeye akiwa Mbunge wa Jimbo, dada yake Mbunge viti maalum, Baba yake Mzee Jabiri Kigoda akiwa diwani wa Kata ya Vibaoni akawa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Handeni.

Lakini pia baada ya uchaguzi wa mwaka 2005, aliona kabisa Wazigua baadhi yao wameanza kumchoka hasa wale waishio Handeni mjini, akaanzisha mchakato wa kuligawa Jimbo mwaka 2008. Akaomba ridhaa mwaka 2010 kwa kutumia ukongwe na utajiri alionao akagombea na mdogo wake Aisha kumshawishi aende Kilindi, yeye alifanikiwa kwa sababu nilizotaja ila dada yake alishindwa vibaya na Mh. Bitrice Shelukindo. Hadi mwaka 2012, alifanikiwa kuligawa Jimbo la Handeni na kupata majimbo mawili MJINI na VIJIJINI.

Ili ujue hasa yote kayafanya kimaslahi jiulize katika mgawanyo wa Handeni na Kilindi nasi kubakia na vitu vingi kama majengo ya Boma, Hospitali na Shule ya Sekondari tumepiga hatua zipi zaidi kiuchumi, kielimu na kiafya ambazo tumemzidi sana mtoto wetu Kilindi?
Leo tuna Halmashauri ya Mji Handeni, hii ndio ilikuwa shida yetu sisi wana wa Handeni? Kumlazimisha mkulima na mfugaji wa MSASA, KWAMASAKA, KWAMAGOME, KILIMILANG'OMBE, KWAMALAHO na MISIMA aishi maisha ya kimjini ya kulipia kodi nyumba yake na ardhi yake lisiwe shamba ila plan ya mipango miji haya ndio ameona yanatufaa sana kuliko kuboresha Hospitali kwa vipimo vyote, dawa na chumba cha kuhifadhia maiti, au kupata maji ya uhakika ya bomba ama kuharakisha kupata "A"levo na chuo cha maana Handeni.

Angalia dhana ya mji wakubwa wote wa Halmashauri ya mji ni rafiki zake wastahafu wa Halmashauri ya Wilaya.
Ifike wakati sasa Handeni tuseme basi! Au yeye mwenyewe kwa kuwa ni Alhaj, aone imetosha sasa kufanya dhuluma Handeni.

-MWISHO POLE WEWE ULIYEUMIZWA NA COMMENT HII- Jumatatu njema!


Huu ni mtazamo binafsi wa mwanaharakati Rashid Kilo kutoka Misima, wilayani Handeni, mkoani Tanga aliyouandika kwenye group la Handeni Kwetu kwenye mtandao wa facebook kwa ajili ya kuzungumza na wadau mbalimbali katika group hilo.
 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...