https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, February 20, 2015

Msanii Mez B afariki Dunia mjini Dodoma alipokuwa akiugua

HABARI ambazo hazijathibitishwa rasmi na familia, zinasema kuwa mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya, Mez B, amefariki Dunia mjini Morogoro baada ya kusumbuliwa na maradhi. Taarifa za kifo cha msanii zimetufikia hivi punde baada ya kufariki. Kifo cha msanii huyo ni pigo katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya.
 
Mwimbaji wa Bongo Fleva, Mez B, enzi za uhai wake.
Mez aliwahi kutamba na nyimbo kadhaa kama ule wa Nimekubali, ambao alipoutoa ulifanya vizuri, bila kusahau nyimbo yake ya kwanza iliyokwenda kwa jina la Kikuku, ambao uliweza kumtambulisha katika tasnia hiyo.

Taarifa zaidi za msiba huo zitaendelea kukujia baada ya kuzungumza na wadau mbalimbali, bila kusahau familia yake na kuelezea pia taratibu zote za msiba huo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...