https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, May 09, 2015

UTT watembelea China kuangalia uwezekezaji na maanufaa yake

kwana Bodi ya UTT-PID ikiongozwa na mwenyekiti wake Mrs. E Mlaki pamoja na Menejimenti wakiwa na wenyeji wao katika jiji la Chengdu ambapo walifanya ziara katika maeneo tofauti ya uwekezaji na manufaa wanayopata wananchi wa jiji hilo. Ziara hiyo ya siku Tano katika Miji tofauti inatarajia kukamilika Tarehe kumi kabla ya kurejea nyumbani.

Na Mwandishi Maalum
Bodi ya Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyo chini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID), pamoja na Menejimenti yake ipo nchini China katika ziara maalum ya Mafunzo na kujenga uzoefu ya siku tano ikiwa na lengo la kuimmalisha utendaji kaziw wa taasisi hiyo.

Katika ziara hiyo, Bodi ya UTT-PID, ikiongozwa na mwenyekiti wake Mrs. E Mlaki pamoja na Menejimenti wapo katika miji mbalimbali na kutembelea maeneo tofauti ya uwekezaji ilikushuhudia manufaa wanayopata wananchi wa maeneo hayo.

Kazi za UTT-PID ni pamoja na Utoaji huduma za ushahuri katika maeneo ya upembuzi yakinifu wa miradi mbalimbali, Uratibu wa fedha na huduma zinazohusiana katika maandalizi ya mapendekezo ya miradi kwa benki au taasisi za fedha, uteuzi wa watoa huduma kuhusiana na maandalizi ya zabuni na usimamizi wa majengo na mali ambao ni utoaji wa huduma fanisi za usimamizi wa majengo yaliyochini ya uangalizi thabiti wa taasisi.

pili
Bodi ya UTT-PID pamoja na Menejimenti ikipata Maelezo kutoka wataalum wa uzalishaji nishati toka mji wa Chengdu.
saba
Pichani Wajumbe wa Bodi ya UTT-PID wakiwa na wenyeji wao ndani ya ukumbi wa mikutano nchini China katika ziara hiyo ya siku 5.
sita
Wajumbe wa Bodi ya UTT-PID wakiwa na wenyeji wao ndani ya ukumbi wa mikutano nchini China katika ziara hiyo ya siku 5.
tano
Mkutano ukiendelea baina ya Wajumbe wa Bodi ya UTT-PID wakiwa na wenyeji wao ndani ya ukumbi wa mikutano nchini China katika ziara hiyo ya siku 5.
tatuBodi ya UTT-PID ikiongozwa na mwenyekiti wake Mrs. Elpina Mlaki (wa pili kushoto) pamoja na Menejimenti wakiwa na wenyeji wao katika jiji la Chengdu ambapo walifanya ziara katika maeneo tofauti ya uwekezaji na manufaa wanayopata wananchi wa jiji hilo.
nne
Wajumbe wa Bodi ya UTT-PID, wakipata maelezo kutoka kwa mtaalamu kutoka Zipingpu Hydropower mwenyeji wao, jinsi gani uzalishaji unavyofanyika na usambazaji wa nguvu za nishati. Mjumbe wa Bodi Mrs. J Mmari (kulia), akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Dr. Gration Kamugisha mwenye shati jeupe na kushoto ni Mwanasheria wa Taasisi hiyo, Bi. Tuzo Mpiluka.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...