https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 01, 2015

Ligi ya Tanzania Bara kuendelea wikiendi kwa Simba kuwavaa Azam, Ndanda kumenmyana na Kagera Sugar



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania bara inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki hii kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini, huku michezo mitatu ikichezwa siku ya jumamosi na michezo mingine mitatu ikichezwa siu ya jumapili.

Jumamosi katika Uwanja wa Sokoine wapinzani wa jiji la Mbeya, Prisons FC watakua wenyeji wa wagonga nyundo Mbeya City mchezo utaochezwa majira ya saa 10 kamili kwa saa za Afrika mashariki na Kati.

Katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona wenyeji timu ya Ndanda SC watawakaribisha wakata miwa wa Kagera Sugar, huku jijini Tanga Mgambo Shooting wakiwa wenyeji wa maafande wa JKT Ruvu mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani.

Jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaa, Simba SC watawakaribisha Azam FC, mchezo ambao unatabiriwa kuwa na upinzani mkali kusaka nafasi ya pili ili mwakani kuweza kuwakilisha Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Jijini Tanga wagosi wa kaya Coastal Union watawakaribisha timu ya Stand United kutoka mjini Shinyanga, mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani, huku kwenye Uwanja wa Manungu mjini Morogoro wenyeji Mtibwa Sugar wakiwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...