https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, May 23, 2015

Mwelekeo wa utalii mkoani Kilimanjaro

Baadhi ya watalii wa ndani wakiwa katika gari kuelekea kilele cha Shira katika hifadhi ya mlima Kilimanjaro.
Kundi la Pili la watalii wa ndani wakiwa katika eneo la uwanda wa Shira mara baada ya kufika kwa usafiri wa gari hadi katika eneo hilo.
Afisa Masoko wa Hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro akizungumza na watalii wa ndani kabla ya kuendelea na safari ya kutembelea vivutio mbalimbali viyoko katika uwanda wa Shira yakiwemo mapango ya Shira Caves.
Safari ya kuelekea katika vivutio vya asili katika uwanda wa Shira ,hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara (MOCU),Faustine Bee akitizama mandhari katika uwanda wa Shira wakati akipanda mlima huo kuelekea katika mapango ya Shira.
Raia wa kigeni wakipata kumbukumbu katika maeneo mbalimbali ya hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro.
Watalii wa ndani wakichukua taswira mbalimbali mara baada ya kufika kilele cha Shira ndani ya Hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara (MOCU) Faustine Bee akichukuliwa taswira na kijaa wake baada ya kufika eneo la Shira hut.
Safari ya kuelekea kutizama mapango ikiendelea.
Watalii wa ndani wengine waliweka kumbukumbu.
Safari ikaendelea.
Baada ya kupanda vilima watalii wa ndani pia walipata nafasi ya kupumzika.
Watalii wa ndani wakiwa katika mapango ya Shira ambayo yalitumiwa na wapagazi wakati wa zoezi la kupandisha watalii wakati wa safafri ya kuelekea kilele cha Uhuru,
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara (MOCU) Prof,Faustine Bee akifurahia mara baada ya kuingia katika mapango ya Shira.
Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Ushirika Prof,Faustine Bee akizungumza jambo kuhusu miamba iliyoko katika mapango hayo.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mwanga wakiongozwa na meneja wao ,Innocent Silayo(wa pili toka kulia) wakishuka mara baada ya kutembelea vivutio  katika uwanda wa Shira.
Mmoja wa watalii wa ndani, Dkt Gaspaer Mpehongwa ,(Kulia) akizungumza jambo na wageni wakati akiwaonesha moja ya picha inayoonesha namna ambavyo volcano ilivyo ripuka na kutengenza uwanda wa Shira.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...