https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, August 26, 2015

Mkuu wa Wilaya Kinondoni, Paul Makonda, azindua tawi jipya la benki ya First National Bank Mbezi Beach jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati) akikata utepe kuzindua rasmi tawi la benki ya First National la Mbezi Beach jana jijini Dar es salaam huku akiambatana na Balozi wa Heshima wa Djibouti Said Shamo na Mkuu wa Huduma za Rejareja wa benki hiyo, Francois Botha.
Mkuu wa Bidhaa na Huduma za Mitandao, Silvest Arumasi akimpa maelekezo Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda mara baada ya kufungua rasmi tawi la benki ya First National la Mbezi Beach jana jijini Dar es salaam. Pembeni yake ni Balozi wa Heshima wa Djibouti Said Shamo.

Mkuu wa Huduma za Rejareja wa benki hiyo, Francois Botha akiongea machache wakati wa ufunguzi rasmi tawi la benki ya First National la Mbezi Beach jana jijini Dar es salaam.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akitoa shukrani zake za pekee kwa benki ya First National kwa kuendelea kufungua matawi yake pembezoni mwa mji wa Dar es Salaam ambapo alisema ni jambo la faraja sana pale mteja anapofuatwa alipo na si kila siku kukimbilia kufungua benki katikati ya mji. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa pili toka kulia) akiwa na Balozi wa Heshima wa Djibouti Said Shamo ( kwanza kulia) pamoja na viongozi wa benki ya First National. Kulia ni Mkuu wa Huduma za Rejareja, Francois Botha na Mkuu wa Bidhaa na Huduma za Mitandao, Silvest Arumasi.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiongea machache na mmoja ya kiongozi wa Benki hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya First National na wageni waliohudhuria uzinduzi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda  akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Huduma za Rejareja wa benki hiyo, Francois Botha.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...