https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, November 30, 2012

Wezi wa Sharomillionea wanaswa Muheza

Na Kambi Mbwana
VITU viliyoibwa vya marehemu Hussein Mkiety, maarufu kama 'Sharomillionea', vimesalimishwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni wezi, waliompora mara baada ya kupata ajali na kupotea uhai wake, katika kijiji cha Songa Kibaoni, wilayani Muheza, mkoani Tanga, mapema wiki hii.

Ajali hiyo ilitokea Jumatatu saa mbili na nusu usiku na kusababisha kifo cha msanii huyo mahiri wa uchekeshaji hapa nchini.
Msanii huyo alitokuwa akitokea jijini Dar es Salaam na kuelekea Lusanga wilayani Muheza kwa ajili wa kuwasalimia wazazi wake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Massawe, alithibitisha kupatikana vitu hivyo ambapo alisema upatikanaji wake ulitokana na msako mkali uliofanya na uongozi wa serikali wilayani Muheza wakishirikiana na Jeshi la Polisi.

Massawe alisema baada ya kutokea kwa tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoani Tanga liliweka mtego na kutangaza kuinunua simu ya mkononi ya msanii huyo aina ya blackberry na ndipo moja kati ya wezi ambao walihusika kwenye tukio hilo walipojitokeza na kuipeleka kwa ajili ya kuiuza na wakati walipofika eneo ambalo walikubaliana walikabidhi simu kwa ajili ya kuikagua na baade wezi hao kushtukia mtego huo na kukimbia huku wakiiacha simu hiyo.

Aidha kamanda Massawe alivitaja vitu ambavyo vimesalimishwa kwa jeshi hilo ni simu ya mkononi aina ya Black Berry, Betrii ya gari, tairi ya akiba, radio ya gari, begi ambalo lilikuwa na nguo za marehemu, saa ya mkononi na nguo ambazo alikuwa amevuliwa sharomilionea na vibaka wa eneo hilo mara baada ya kutokea ajali hiyo.

Kamanda Massawe alisema mpaka hivi sasa hakuna mtu yoyote anashikiliwa na jeshi la polisi kufuatia kutokea kwa uporaji huo huku Jeshi hilo likiendelea na uchunguzi ili kuwabaini waporaji hao na kuweza kufikishwa katika vyombo vya sheria ili kuweza kujibu tuhumu zinazowakabili na kutoa wito kwa wananchi kuacha kufanya vitendo vya uporaji pindi ajali zinapotokea katika maeneo yao.

"Tupo kwenye uchunguzi mkali ili kuhakikisha tuwatia mbaroni wale wote ambao waliohusika na kitendo cha kinyama alichofanyiwa msanii huyo alisema "Kamanda Massawe.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...