https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, November 29, 2012

Tunda Man anywea mazishi ya Sharomillionea



 
Picha mbalimbali za mazishi ya msanii Sharomillionea, Muheza Tanga





Na Kambi Mbwana, Muheza
MWIMBAJI wa muziki wa Bongo Fleva, Tunda Man, katika muda wote wa msiba wa Hussein Mkiety, maaruru kama Sharomillionea, alikuwa amenywea, wakati wote akiwa kimya, hivyo kuonyesha alikuwa kwenye mawazo makubwa.

Kuanzia katika Hospitali ya Teule Muheza ulipokuwapo mwili wa msanii Sharomillionea, Tunda Man anayetokea katika kundi la Tip Top Connection hakuweza kusema lolote, zaidi ya kupepesa macho yake kwa majonzi.

Baada ya kumaliza taratibu za mazishi ya Sharomillionea, msanii huyo aliyekuwa kwenye uswahiba na marehemu, alisema kuwa hakujisikia vizuri kwa kushuhudia msanii mwenzake amelazwa chumba cha maiti na baadaye kaburini.

“Ni mbaya sana kuangalia kuona mtu uliyechat naye muda uliopita, au ulikuwa naye wakati Fulani anaingizwa kaburini na kubadilishwa jina lake kirahisi namna hii.

“Nimeumia sana kwa msiba wa Sharomillionea, lakini sisi binadamu ni watu wa kupita hapa duniani zaidi ya kuombeana kwa Mungu maana huwezi jua nani anafuata nyayo baada ya leo kutoka hapa nyumbani kwa Sharomillionea,” alisema Tunda Man.

Tunda Man anatokea katika kundi la Tip Top Connection lenye mjumuiko wa wasanii mahiri, akiwamo kiongozi wao Ahmad Ally ‘Madee’, anayejiita pia Rais wa Manzese.




No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...