https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, November 29, 2012

Mkuu wa wilaya Muheza awakera wengi



Na Kambi Mbwana, Muheza
MKUU wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, jana aliwakera watu wengi waliovamia hospitali ya Teule kwa ajili ya kuangalia jinsi msanii Hussein Mkiety, maarufu kama Sharomillionea anavyoandaliwa kwa ajili ya kuzikwa kijijini kwao Lusanga, wilani Muheza, mkoani Tanga.

Kabla ya hapo, baba mkubwa wa Marehemu, aliweka utaratibu wa baadhi ya ndugu na jamaa kushiriki kwa karibu kuandaa mazishi ya msanii huyo aliyefanya vyema katika sanaa hapa nchini.


“Haiwezekani jamani watu wote mliokuwapo hapa kuingia katika chumba cha kuhifadhia maiti badala yake wote tuhamie nyumbani kwao kwa ajili ya kuzika na sio kuminyana hapa.

“Naamini uamuzi huu ni mbaya na unakera kwa kiasi kikubwa, lakini lazima mjuwe kuwa naongea hapa kama mtu wa serikali na itakuwa vyema kama mashabiki na wakazi wote wa Tanga tutaelewana katika hilo,” alisema Subira huku akiangaliwa vibaya na wananchi.

Kauli ya Mkuu huyo wa Wilaya ya Muheza, ilifuatiwa na amri ya jeshi la Polisi kuwazuia watu kuendelea kuingia katika upande wa chumba cha kuhifadhia maiti.

Idadi kubwa ya mashabiki na wasanii walikuwa wengi katika wilaya ya Muheza kuangalia namna gani kijana wao mpendwa anaingizwa katika nyumba ya milele baada ya kufariki kwa ajali ya gari karibu na kijiji chao cha Lusanga.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...