https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, November 26, 2012

Wazee wa Ngwasuma kuvamia Morogoro Ijumaa



 Rais wa FM Academia, Nyosh El Sadaat
 
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya muziki wa dansi ya FM Academia, maarufu kama Wazee wa Ngwasuma, inatarajia kufanya onyesho la nguvu katika uzinduzi wa pub ya ‘Babylon’, iliyopo Kilosa, mkoani Morogor kwa ajili kiwanja hicho kipya cha burudani.

Ngwasuma wanafanya shoo hiyo wakiwa na lengo moja la kuonyesha makali katika ramani ya muziki wa dansi hapa nchini, huku wakiwa na wakali mbalimbali wanaofanya makubwa katika mustakabali wa bendi hiyo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa ukumbi huo, Daudi Mfaume, alisema kwamba maandalizi ya kuwaleta wakali hao katika mji wao huo yamekamilika, huku wakiamini kuwa mashabiki wao watapata makubwa.

Alisema kuwa Ngwasuma wamekuwa na mashabiki wengi katika mji wa Morogoro, hivyo kwakuwaleta Kilosa, mashabiki wao watapata kitu adimu na kuweka historia kamili katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini.

“Tumepanga kuwaleta wakali wa muziki wa dansi hapa nchini, Wazee wa Ngwasuma kwa ajili ya kuwapatia burudani mashabiki wao watakaoingia katika uzinduzi huo wa Babylon wakiwa kama wadau na mashabiki wa muziki nchini.

“Naamini kila kitu kitakwenda sawa, hivyo wadau na mashabiki wa muziki wa dansi wa mkoani Morogoro, wajiandae kwa ajili ya burudani hiyo itakayofanyika katika ukumbi mpya wa burudani katika mji wetu wa Kilosa,” alisema Mfaume.

Wazee wa Ngwasuma ipo chini ya Rais wa Vijana, Nyosh El Sadaata, akiwa sambamba na waimbaji wengine nguli, akiwamo Patchou Mwamba, ambaye pia anatamba katika tasnia ya filamu, baada ya kucheza filamu mbalimbali zinazokubalika nchini.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...