https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, July 15, 2016

Mkuu wa Mkoa Mbeya akabidhi Power Tiller 102 alizopokea kutoka kwa mbunge wa Mbarali

Na Mwandishi Wetu, Mbeya
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla amepokea power Tiller 102 zenye thamani ya shilingi milioni 510 kutoka kwa mbunge wa jimbo la Mbarali mhe Haroun Mulla kwa ajili ya shughuli za kilimo na kijamii kwa Vijiji na mitaa 102 ya jimbo la Mbarali.
Mkuu wa Mkoa Mbeya, Amos Makalla akizungumza jambo baada ya kukabidhi Power Tiller zenye thamani ya Sh milioni 510 kutoka kwa mbunge wa Mbarali.
Akikabidhi msaada huo mbunge wa jimbo hilo amesema kuwa wilaya ya mbarali ni wilaya ya kilimo na ufugaji hivyo msaada wake umelenga kusaidia Vijiji na mitaa ili kuchochea Vijiji na mtaa kuwa na chanzo cha mapato na pia kuchochea kilimo. Akipokea kabla ya kuzikabidhi power tiller hizo kwa viongozi wa Vijiji na mtaa amemshukuru na kumpongeza mbunge kwa msaada huo mkubwa na kwa kufanya hivyo ametekeleza vizuri ilani ya Chama tawala ya kuongeza ajira akiamini hizo power Tiller zitaendeshwa na madereva na wasaidizi na pia zitaongeza ukuaji wa uchumi.
Power Tiller pichani.
Aidha amewataka viongozi wa Vijiji kuzitunza na kueleza kwa wananchi mapato yatakayopatikana kutokana na hizo power tiller." Siyo hizi power tiller ziwe Mali zetu ni Mali za kijiji mzitumie vizuri na tuache fitna maana kuna wengine wangetamani badala ya powe tiller mngepewa Fedha hapa nasema Mbunge katupa nyavu tukavue siyo Samaki nawatakia kazi njema na Mipango mizuri"
Amewataka wananchi wote kufanya kazi na muda kwa vijana kucheza pool haupo na hivyo halmashauri zote zitenge asilimia 5 a mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya vijana na akina mama

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...