https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, July 15, 2016

Mkutano wa kuombea Taifa amani kuanza Julai 19

 Mwenyekiti wa Good News for All Ministtry (Great Vition 2000), Askofu Dk.Charles Gadi (wa pili kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu mkutano mkubwa wa kuombea Taifa kila Jumanne kwa siku 1001 utakaofanyika kuanzia Julai 19, 2016 viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mchungaji James Manyama, Palemo Massawe na Mchungaji Leonard Kajuna.


Na Dotto Mwaibale



Mwenyekiti wa Good News for All Ministtry (Great Vition 2000), Askofu Dk.Charles Gadi anatarajiwa kuongoza mkutano mkubwa wa kuliombea Taifa utakaofanyika kuanzia Julai 19 katika viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ametajwa kuwa mgeni rasmi wa mkutano huo.


Makonda anatarajiwa kuzindua mkutano huo wa maombi hayo ya siku 1,001 ambayo  yataendelea kufanyika siku ya Jumanne ya kila wiki.


Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkutano huo 

Dar es Salaam leo, Askofu Dk. Charles Gadi alisema maandalizi ya  maombi hayo yamekwisha kamilika na kuwa yanakuja kufuatia mengine ya siku elfu moja na moja ya kuliombea taifa yaliyokwisha kufanyika  mwaka 2012 na kukamilika mwaka 2015.
 Mchungaji Palemo Massawe (kulia), akitoa ufafanuzi kwa wanahabari kuhusu mkutano huo.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Askofu Dk. Charles Gadi (wa pili kushoto), na wachungaji wenzake wakiomba baada ya kuzungumza na wanahabari.




Alisema "Tunakumbuka tulianza maombi ya siku elfu moja mwaka 2012 ambapo yalitimiza mwaka 2015, tunashukuru Mungu kwamba yote tuliyoyaorodhesha katika mahitaji ya siku hizo 1,001 yametimizwa na mengi yako mbioni kutimizwa". 



Alisema katika siku 1,001 wanakusudia kuombea mambo 16 yakiwemo kuombea wananchi wawe na utayari wa  kulipa kodi, kuhamasisha wanachi kujiunga na mifuko ya jamii, watunze na kulinda miundombinu ya taifa, matumizi endelevu ya ardhi, kuhamasisha utalii wa ndani, wananchi kupenda kupima afya zao mara kwa mara na wawe na tabia ya kujiwekea kumbukumbu ya hesabu ya shughuli zao.


"kuhamasisha  wananchi kulinda maadili ya taifa, kuhamasisha usafi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla, kuhamasisha wanachi kupenda vitu vya hapa nchini, kuiomba serekali iwalinde na kuwawezesha wawekezaji wa ndani na kuiombea serekali iweze kununua vifaa vya kutomsha kwa ajili ya hospitali zetu " Alisema


Askofu Dk. Gadi alitumia muda huo kuwaomba wananchi na waumini wengine kutoka madhehebu na dini mbalimbali kujitokeza kwa wingi katika mkutano huo ambao ni muhimu wa kuliombea taifa la Tanzania liendelee kuwa na amani ili watu wake waweze kuendelea kufanya shughuli zao za kiuchumi.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...