https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, September 28, 2011

Tatizo la maji Kilwa lapatiwa ufumbuzi






                                                       
Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu juu na Mustafa Sabodo, mfanyabiashara chini.


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MFANYABIASHARA maarufu Mustafa Sabodo na Mtanzania anayeishi nchini Marekani, Faraja Ukondwa, wameahidi kuchimba visima vya maji safi na salama 133, wilayani Kilwa, hivyo kupunguza tatizo la uhaba wa maji linaloyakumbuka maeneeo mengi mjini humo.

Hayo yamesemwa na mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), jijini Dar es Salaam jana, alipokuwa akizungumza na Mtanzania kuhusiana na kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wake.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mangungu mmoja wa wabunge machachari waliopita katika uchaguzi wa mwaka jana, alisema kwa kupitia msaada huo, wananchi wa Kilwa watanufaika na maji hayo, mara baada ya visima 30 kutoka kwa Sabodo na visima 100 msaada wa Ukondwa, kukamilika.

Alisema kero ya ukosefu wa maji ni kubwa katika maeneo hayo, hivyo kujitokeza kwa watu hao ni dalili njema za kuanza kufanyia kazi matatizo yanayowakabili wananchi wote na wakazi wa Kilwa.

“Nimekuwa katika presha kubwa kutafuta namna ninavyoweza kusaidia maendeleo katika jimbo langu na maeneo yote ya Kilwa, hivyo kujitokeza kwa wafanyabiashara hao kutapunguza matatizo hayo.

“Naamini wananchi wote watafaidika na maji hayo, hivyo ni jukumu la kila mwenye uwezo wake kushirikiana kwa karibu kutafuta namna tunavyoweza kuwakomboa watu wa Kilwa wenye utajiri mkubwa, japo kuwa wanaishi katika umaskini wa kutupwa,” alisema Mangungu.

Kwa mujibu wa Mangungu, yupo kwenye hatua za mwisho za kufanya ziara katika maeneo yote ya jimbo lake, akiwa na nia ya kuangalia jinsi ya kuweza kukabili changamoto kwenye eneo lake.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...