https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 30, 2011

Wakali wa Ulaya walivyotoana jasho







MICHUANO ya klabu Bingwa Ulaya iliendelea tena Jumanne na Jumatano katika viwanja mbalimbali barani Ulaya.

Katika mechi za Jumanne Manchester United ikiwa nyumbani ilitoka sare ya mabao 3-3 na Basel FC ya Uswisi.
Dany Welbeck alipachika mabao mawili ya haraka dakika ya 16 na 16……………., lakini Fabian Frei alifunga bao kipindi cha pili kabla ya kaka yake, Alexander Frei akufunga mengine mawili na kuwaweka mbele, lakini Ashelay Young alisawazishia United.

Mechi nyingine ilikuwa ni kati ya Bayern Munich dhidi ya Man City katika Uwanja wa Allianz Arena, ambapo mabao mawili ya Mario Gomez yaliilaza City.
Trabzonspor walitoka sare ya bao 1 – 1na  Lille, Real Madrid wakiwa nyumbani waliichapa Ajax mabao 3 – 0 yakifungwa na Ronaldo, Kaka na Karim Benzema.

Otelul Galati wa walifungwa na Benfica nyumbani bao 0-1,  Napoli          waliishinda mabao 2 – 0 dhidi ya Villarreal,
Lyon wakaibanjua 2 - 0 Dinamo Zagreb na Inter Milan waliifunga CSKA Moscow 2 – 3.

Kwenye mechi za Jumatano Chelsea walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Valencia, bao la Chelsea lilkuwa la kwanza likifungwa na Frank Lampard kabla ya  Soldado kusawazisha kwa penalty.
Arsenal ambao msimu huu wamekuwa hawapewi nafasi kubwa kutokana na kuanza vibaya kwenye Ligi ya England, wameichapa Olympiacos mabao 2-1, bao la kwanza lilifungwa na Alex  Oxlade-Chamberlain dakika ya 7 na la pili lilipatikana dakika ya …………………………….. Andre Santos (19),  David Fuster aliipatia timu yake bao la kufutia machozi dakika ya 26.

Shakhtar Donetsk walitoka sare na 1 – 1 Apoel Nicosia, Marseille          waliichapa mabao 3 - 0   Borussia Dortmund, Bayer Leverkusen ilishinda 2 – 0 dhidi ya Genk na Zenit St Petersburg waliizamisha FC Porto mabao3 – 1.

BATE walikula kichapa cha mabao 5 –0 kutoka kwa Barcelona, mchezaji wa BATE alianza kujifunga dakika za mwanzo, Messi aliweka nyavuni mara mbili, Pedro na Villa kila mmoja akifunga moja.
AC Milan waliifunga 2 - 0    Plzen, Ibrahimovic na Cassano waliipatia ushindi huo klabu hiyo yenye makazi yake San Siro.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...