https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 30, 2011

Mjuwe Marlaw kifaa cha Besta





Marlaw akiwa na Bestaaaa


BABA mwimbaji, mama mwimbaji – tazama familia hii, kama atapatikana mtoto itakuwaje?
Swali kama hilo pia unaweza kujiuliza kuhusu Beyonce Knowles na mumewe Shawn Carter ‘Jay-Z’.
Lakini, katika jukwaa la muziki wa Tanzania, hasa wa kizazi kipya, naizungumzia familia iliyoanzishwa na Marima Lawrence na Besta Rugeiyamu.
Wawili hao ni wanandoa na pia ni waimbaji mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, wakati mume akijulikana vyema na mashabiki wake kama Marlaw na mke akitambulika kwa jina la Besta.
Unadhani akipatikana mtoto kwenye familia hiyo atarithi kitu gani? Kwa haraka utasema ni muziki, na kuzitazama kama familia ya Will Smith na mkewe Jada Pinkett – ambao watoto wao, Jayden na Willow, wanatesa kwenye muziki na filamu kama ilivyo kwa wazazi wao.
Mkali huyo alitupasha kuwa yote juu ya ndoa yake na masuala mazima ya muziki.
Tanzania inamtambua Marlaw kutokana na kujishirikisha na sanaa ya muziki, lakini malengo ya mwimbaji huyo ni kuufikisha mbali muziki wake, ikiwa pamoja na kutambulika katika bara zima la Afrika.
Wakati akiwa na fikira hizo, Marlaw anatambua ujio wa waimbaji wapya ambao wanaongeza ushindani katika tasnia hiyo hapa nchini.
“Kuongezeka kwa wasanii kunazidisha ushindani na kuibua changamoto mpya katika muziki,” anasema.
Muziki umekuwa ni sehemu ya maisha kwa msanii huyo, tofauti na ilivyokua mwanzo wakati anaanza kufanya kazi hiyo.
Marlaw, ambaye alikuwa msanii kutoka Tanzania House Of Talent (THT), alijiunga katika jumba hilo la vipaji kwa ajili ya kujiongeza ujuzi zaidi baada ya kuachia kibao chake cha Bembeleza mwaka 2007.
Marlaw alijifunza mambo mengi THT, ukiachilia uimbaji, pia aliweza kujifunza namna ya ‘kuperform’  na bendi ‘live’.
Baada ya kuachia Bembeleza, msanii huyu alikaa kimya kwa muda akijipanga upya na kuachia nyimbo nyingine kibao kama Rita, Daima na Milele, Bado Umenuna aliyomshirikisha Chid Benzi na Pii Pii (Missing my Baby).
Marlaw anatamba katika soko la muziki na albamu zake mbili ya kwanza ikiwa ni Bembeleza na ya pili ni Bidii.
Albamu ya Bembeleza iliitoa Septemba (2007) ikiwa na nyimbo (12), ambazo ni Bembeleza, Rita, Bado Umenuna, Daima na Milele, Busu la Pink, Si mimi.
Wakati ile ya Bidii iliyoitoa Septemba (2009) ilikuwa na nyimbo 12 pia,  zikiwemo Pii Pii (Missing my Baby), Sorry Sana, Be Happy na Tanzania.
 Msanii huyo alikutana na mkewe, Besta kwenye muziki wakawa na uhusiano, huku wakiendelea na tasnia hiyo hadi walipoamua kufunga ndoa ili kuwa mke na mume.
Akizungumzia juu Serikali kusaidia sanaa hiyo ya muziki, Marlaw anasema kuwa iko tayari kusaidia na ndio maana imeanza na msaada wa studio ya ‘mastering’, kitu ambacho ni muhimu sana kwa kazi zetu.
Pia alizungumzia muziki wa nje na ule wa kwetu akisema muziki wa nje una maendeleo mazuri, kwa kuwa wana mifumo madhubuti kwenye pande zote za haki ya sanaa kuanzia usambazaji wa kazi, haki miliki na hata matumizi ya sanaa kiujumla.
Kwa sasa unapomzungumzia Marlaw ni kama unauzunguzia muziki, kwa sababu chakula chake anakipata kutokana na kufanya muziki, makazi yake anayolala yanatokana na ujira anaopata kwenye muziki, lakini kubwa kwenye mapenzi – mkewe ni mwimbaji.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...