https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 30, 2011

Sumalee mdheee wa Hakunagaaa


HAKUNAAGA zaidi yangu mi na wewe, hakunaaga zaidi yangu mi na wewe, hakunaaga zaidi yangu mi na wewe, hakunaaga zaidi yangu mi na wewe, hakunaaa, hakunaga, hakunaaa hakunaga.
Hiko ni kiitikio cha wimbo mpya wa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Suma Lee, uitwao Hakunaga, kibao ambacho kimepigwa katika mahadhi ya kwaito.
Wimbo huo tayari umeanza kuwabamba mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva na kupata Air Time katika vituo mbalimbali vya redio, huku video ya wimbo huo ukifanya vizuri pia.



Sumalee akiwa katika picha tofauti...
Sasa mkali huyo anatamba na wimbo wake wa 'Hakunaga'
Msanii huyo alianza masuala ya muziki kwa mara ya kwanza mwaka 2000 na moja kwa moja akaingia studio na kutoa wimbo ulioitwa Sivuti na Mama, akiwa na kundi la Parklane lililokuwa na makazi yake mjini Tanga.
Hakuweza kufanya muziki kabla ya hapo kwa kuwa familia yake haikuwa tayari kumuacha ajiingize katika masuala hayo, lakini muda ulipofika yeye mwenyewe aliamua liwalo na liwe.
Ingawa hakuwahi kufanya muziki kabla ya hapo, lakini aliweza kuingia studio, ambapo mwaka huo waliweza kutoa wimbo mwingine uitwao Aisha, wakati huo C Pwaa alikuwa amejiunga na kundi hilo la Parklane.



Baada ya Parklane kusambaratika, wasanii waliounda kundi hilo kila mmoja alijishughulisha na muziki binafsi.
Suma Lee, ambaye jina lake halisi ni Ismail Thabit, aliyezaliwa Tanga katika Hospitali ya Mkoa ya Bombo, mwaka 2006 alitoka kivyake na kibao kiitwacho Chungwa.
Wimbo huo uliweza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio, huku ikishika katika chati za vituo hivyo vya redio hapa nchini na nje ya mipaka yetu.
Suma alitoa albamu ambapo wimbo huo wa Chungwa ndio ulibeba jina la albamu, zikiwemo nyimbo nyingine kama Rafiki, Chaguo Lake, Gomba na Ba na Ma.
Kutoka kwa kibao cha Hakunaga ni maandalizi ya albamu yake mpya baada ya ile ya kwanza ya Chungwa.
Albamu hiyo mpya itakayoitwa Hesabu za Mapenzi itakuwa na nyimbo 15, ukiwemo wimbo mkali uliofanya vizuri mwaka 2009 uitwao Ndani One Week.
Katika albamu hiyo mpya kutakuwa na nyimbo kama
Nikueleze, Uk Dubai, Aunt na Hakunaga pamoja na Ndani One Week ambazo tayari ameshaziachia.
Suma Lee amekuwa na utaratibu wa aina ya pekee tofauti na wasanii wengine, kwani huchukua muda mrefu hadi kutoa ‘single’ moja hadi nyingine.
Singo ya mwisho Suma Lee kutoa ilikuwa ni Ndani ya One Week, ambayo ilikuwa mwaka 2009 na kufanya vizuri, hivyo ni takribani miaka miwili imepita ndio ametoa Hakunaga.
Akitoa sababu za kuchelewa kutoa singo baada ya kutoa moja, amesema huo ni utaratibu wake, kwani akifanya haraka mashabiki wake watamchoka kama wanavyochokwa wengine.
“Wimbo wangu mmoja ukiusikiliza leo, ndivyo utakuwa na utamu ule ule utakapousikia tena baada ya miaka 10 kupita,” anasema nyota huyo.
Tangu msanii huyo aanze muziki kwa mara ya kwanza mwaka 2000 hadi leo 2011 ni miaka 10 imepita, lakini bado ameonyesha uwezo aliokuwa nao zamani.
Ni miaka 10 sasa tangu aanze sanaa, lakini bado uwezo wake wa kutunga mashairi na kuimba ni wa kipekee na ndiyo maana anaweza akakaa miaka miwili bila ya kutoa wimbo na akija kutoa unakuwa mkali.
Kwa sasa Suma Lee ana mpango wa kutafuta vijana wenye sauti za ukweli na wenye uwezo wa kuimba na kuweza kuinua vipaji vyao.
‘Project’ hiyo ya kuibua vipaji na kuviendeleza ameipa jina la Voice of Suma, ikilenga wale wasanii wadogo wenye sauti nzuri na uwezo wa kuimba kama yeye.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...