https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, December 19, 2016

Viwangp vya watoto wachezao mchezo wa golf vyazidi kupanda

Na Luteni Selemani SemunyuViwango vya Watoto wanaocheza mchezo wa golf katika klabu ya Jeshi la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania ya Lugalo vinazidi kupanda na kuongeza uwezekano wa  kupata vipaji vipya  na Wawakilishi wa Taifa.
Mshindi wa mashindano maalum ya watoto yaliyoandaliwa na klabu ya Golf ya JWTZ ya Lugalo, Habiba Likuli akipiga mpira huku wachezaji wenzake wakimuangalia katika hekaheka za mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Luteni Selemani Semunyu)

Hayo yalisemwa na Mmoja wa Walimu wa Mchezo huo wa Klabu ya Lugalo Elias Chiundu mara baada ya mashindano ya Watoto yaliyofanyika mwishoni mwa Wiki katika Uwanja wa Golf wa Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waaandishi wa habari mwalimu huyo alisema yeye kama Mwalimu anafarijika kwa kuona viwango vya watoto hao vikikua na hivyo ni matarajio yake katika mwaka 2017 watafanya vyema Zaidi.
Mshindi wa pili wa mashindano maalum ya watoto yaliyoandaliwa na klabu ya Golf ya JWTZ ya Lugalo, Sophia Juma, akipiga mpira huku wachezaji wenzake wakimuangalia kwenye mashindano hayo.

“Mwaka 2017 tunataraji baadhi ya watoto  waliokuwa wanacheza katika Daraja la Junior kutokana na Umri wao kuongezeka sambamba na kiwango cha uchezaji basi wataingia katika Divisheni Nyingine na kutoa changamoto kwa waliowakuta” Alisema Chiundu.
Aliongeza kuwa kuna Faida kubwa kwa Wachezaji kuandaliwa wangali wadogo kwani wanakuwa na kipindi kirefu cha  mafanikio iwapo wataweka jitihada sambamba na kuungwa mkono na wazazi.


Katika mashindano hayo mshindi wa kwanza  baada ya kucheza Viwanja 18 aliibuka  Habiba Likuli baada ya kupata  mikwaju ya jumla 89 kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 15 na hivyo kuibuka na Mikwaju ya Jumla 72 akifuatiwa na Sophia Juma aliyepiga Mikwaju ya Jumla 74.

 Mbali na Viwanja 18 pia katika kundi la Watoto waliocheza viwanja Tisa mshindi ni Abra Bella aliyepiga mikwaju ya jumla 48 na katika viwanja vitatu mshindi ni Salehe Ramadhani aliyepiga mikwaju ya jumla 17.

Kwa upande wake mshindi wa mashindano hayo ya siku moja Habiba Likuli amesema mashindano yalikuwa mazuri licha ya changamoto ya jua kuwa kali na kuomba Wazazi  kuwaruhusu watoto wao kuja kushiriki nao ili kuonyesha vipaji na kutumia muda wao vizuri. Jumla ya wachezaji 32 wameshiriki katika mashindano hayo yenye lengo la kupima ukuaji wa vipaji vyao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...