https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, January 08, 2016

Mbwana Samatta aiweka kileleni Tanzania kwa tuzo ya mwanasoka bora

Na Mwandishi Wetu, Nigeria
NYOTA wa kusukuma kabumbu wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Kongo kwenye klabu ya TP Mazembe, Mbwana Samatta, usiku wa kuamkia leo, Abuja nchini Nigeria, ameibuka na tuzo ya mchezaji bora kwa wachezaji wanaocheza Barani Afrika.
Mbwana Samatta, akiwa uwanjani kwenye timu yake ya TP Mazembe.
Tuzo hiyo inazidi kumuweka katika nafasi nzuri mchezaji huyo aliyeibukia katika timu ya Mbagala Malket, African Lyon, Simba SC na sasa TP Mazembe. Watanzania wengi wamekuwa wakielezea hatua hiyo kama sehemu ya kuonyesha furaha yao kutokana na kijana huyo mdogo kuiweka nchi katika kilele cha mafanikio.


Samatta alitangaza saa chache kabla ya fainali hizo kuanza, kuwa ana uhakika mkubwa wa kushinda kwenye tuzo hizo kutokan na nafasi yake nzuri ya kucheza akiwa kwenye klabu yake ya TP Mazembe.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...