https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, June 23, 2017

Muuza simu Dodoma ajazwa Milioni 20 za Biko

MILIONI 20 NYINGINE KUPATA MWINGINE JUMAPILI HII
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MFANYABIASHARA wa simu za mikononi mjini Dodoma, Ramadhan Juma Hussein, jana amejazwa Sh milioni 20 zake alizoshinda kutoka kwa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko, aliyoshinda katika droo ya 16, iliyochezeshwa Jumatano iliyopita.
Mshindi wa droo ya 16 ya Sh Milioni 20 kutoka Biko, Ramadhan Juma Hussein katikati akiwa amebeba fedha zake alizokabidhiwa jana na waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko mjini Dodoma katika benki ya NMB. Kulia ni Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven.
Kupokea kwa pesa zake kumekuja baada ya kuwa miongoni mwa Watanzania lukuki wanaocheza bahati nasibu ya Biko kuwania zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni 1,000,000, pamoja na donge nono la Sh Milioni 20 linalotoka Jumatano na Jumapili.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kulia akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 20 mshindi wao wa Dodoma, Ramadhan Juma Hussein. Wengine wanaoshuhudia ni familia ya Ramadhan wakati wa makabidhiano hayo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika katika benki ya NMB mjini Dodoma, Juma anasema kwamba pesa hizo atazitumia vizuri katika kukuza biashara zake kama alivyokuwa akimuomba Mungu aweze kushinda mamilioni ya Biko.

Ramadhan Juma Hussein akiwa kwenye fyraha baada ya kukabidhiwa jumla ya Sh Milioni 20 kutoka kwa waendeshaji wa Bahati Nasibu ya Biko. Makabidhiano hayo yalifanyika jana katika benki ya NMB Mjini Dodoma.

“Nashukuru nimekuwa mchezaji mzuri wa Biko na huwa nashinda mara kwa mara zawadi za papo kwa hapo ambazo hupatikana kwa kufanya miamala kwenye simu za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba ya kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456.
“Binafsi ninawaamini Biko kwa sababu si mara ya kwanza kushinda zawadi za papo kwa hapo, hivyo nawaomba Watanzania wenzangu tujitokeze kwa wingi kucheza Biko ili tushinde zawadi mbalimbali ikiwamo hii ya Milioni 20 ambayo leo nimekabidhiwa, huku nikiahidi kuwa nitaendelea kucheza Biko zaidi na zaidi,” Alisema.
Naye Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwamba wanaendelea kusambaza mamilioni kutoka kwa washindi wao mbalimbali wanaojitokeza kwa wingi kucheza bahati nasibu yetu rahisi katika uchezaji wake.
“Huu ni wakati wa kulala masikini na kumka tajiri kwa sababu kwa kupitia Biko kila mtu anaweza kuvuna mamilioni yetu ya papo kwa hapo pamoja na donge nono la Sh Milioni 20 linalotoka kila Jumatano na Jumapili,” Alisema.
Biko ni mchezo wa bahati nasibu uliojizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania kwa siku chache tangu kuanzishwa kwake, huku kwa mwezi Mei pekee zaidi ya Sh Milioni 500 zikiwa zimekwenda kwa washindi waliobuka katika nafasi mbalimbali za ushindi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...