https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, October 01, 2011

Kago kwaheri Simba


WAKATI klabu ya Simba, ikitarajiwa kuanza mazoezi leo kwa ajili ya kujiandaa zaidi na mechi za ligi kuu, mshambuliaji wa Kimataifa, Gervas Kago, ameombwa na nchi yake kwenda kujiunga na timu yake ya Taifa.

Hiyo ni baada ya Afrika ya Kati, kuwasilisha barua yao jana, wakati tayari alishajua kuwa ataanza mazoezi na wenzake, licha ya nyota wanne wa Simba, kuitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars, kinachonolewa na Mdenmark, Jan Poulsen.

Wachezaji hao wa Simba walioingia kambini wakijiandaa na safari yao ya Morocco, ni Juma Kaseja, Juma Nyoso, Victor Costa na Amir Mafta.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa kupokea barua hiyo kunaonyesha kuwa naye hatajiunga na wenzake kwa ajili ya kujiandaa na patashika ya ligi ya Vodacom.

Simba wanaendelea na mikakati yao wakati Yanga wao wamesimama mazoezi kwa ajili ya kupisha maandalizi ya Stars, kitu kilichomfanya kocha wao, Mganda, Sam Timbe, kurudi kwao kwa muda.

                               Gervas Kago
“Tunashughulikia usafiri wao kuanzia sasa, nadhani naye hatakuwapo kwenye timu yetu kwa ajili ya kuwakilisha Taifa lake, Afrika ya Kati.

“Ni jambo zuri mchezaji kuwamo kwenye kikosi cha timu ya Taifa, hivyo wale wote ambao hawapo kwenye timu zao za Taifa, kesho (leo) wataanza mazoezi,” alisema Kamwaga.

Simba inaongoza ligi ikiwa na pointi 18, ikifuatiwa na Azam FC yenye pointi 15, wakati Yanga wao wana pointi 12, wakizinduka katika mechi mbili zilizopita na kuonyesha kiu ya kutaka kutetea ubingwa wao huo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...