https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 26, 2017

Mwakaboko: Milioni 10 za Biko zinanikomboa kiuchumi


Meneja Masoko wa Biko Goodhope Heaven kulia akimkabidhi jumla ya Sh Milioni 10 mshindi wa droo ya nane ya Biko, Daniel Dancan Mwakaboko aliyetangwa Jumatano ambapo jana alikabidhiwa fedha zake katika benki ya NMB jijini Dar es Salaam. Kushoto ni afisa wa NMB aliyesimamia zoezi la kuingiza fedha hizo katika akaunti ya mshindi huyo wa Milioni 10 na Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko Grace Kaijage.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MSHINDI wa droo ya nane ya Bahati Nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’, Daniel Mwakaboko, jana amepokea fedha zake jumla ya Sh Milioni 10, huku akisema kuwa zawadi aliyoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko itamkomboa kiuchumi na kumuondoa kwenye hatari ya umasikini inayowakumba vijana wengi.


Akizungumza jana katika makabidhiano ya fedha zake, Mwakaboko alisema kwamba zawadi ya fedha taslimu Sh Milioni 10 ni nyingi kwa wakati huu anaposaka maisha bora kwa kutafuta mtaji mara kadhaa bila mafanikio.
Meneja Masoko wa Biko Goodhope Heaven kulia akimkabidhi jumla ya Sh Milioni 10 mshindi wa droo ya nane ya Biko, Daniel Dancan Mwakaboko aliyetangwa Jumatano ambapo jana alikabidhiwa fedha zake katika benki ya NMB jijini Dar es Salaam.
Alisema kwa sasa anafanya kazi ya kuchapisha majarida na vitu tofauti tofauti vya kiofisi katika ofisi ya mtu mwingine, hivyo ni wakati wake wa kuangalia namna gani atazitumia vizuri fedha za ushindi alizokabidhiwa baada ya kuibuka na ushindi kartika droo ya nane ya Biko iliyochezeshwa Jumatano.


“Biko ni mchezo mzuri usiochosha na unaoweza kumpa kila mmoja wake ushindi kwa sababu hata uchezaji wake wa kuweka muamala kwa simu za Tigo Pesa, MPESA na Airtel Money kwa kuanzia Sh 1000 na kuendelea ni rahisi maana unachotakiwa ni kuingiza namba ya kampuni 505050 na kumbukumbu 2456 tayari kusubiri zawadi ya papo kwa hapo au droo kubwa ya Sh Milioni 10.


“Nina ndoto ya kufanikiwa kiuchumi lakini pia sitahasahau kiwanja maana vitu vyote hivi vilikuwa vikisisumbua kwa siku nyingi na nadhani Mungu amejibu maombi yangu maana hapo kabla hali yangu ilikuwa ngumu,” Alisema Mwakaboko mkazi wa Tabata na mwenye asili ya mkoani Mbeya.

Naye Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwamba kampuni yao imejipanga ipasavyo kuhakikisha kwamba kila mtu anavuna mamilioni ya Biko kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni Moja ambayo hulipwa papo kwa hapo dakika chache baada ya mshindi kupatikana.

“Nawaomba Watanzania wote bila kuangalia unapatikana eneo gani la Tanzania kucheza Biko mara nyingi zaidi ili kujiwekea mazingira mazuri ya ushindi na kupata suluhu ya changamoto za kimaisha kwa kupitia mchezo wa Biko maarufu kama Nguvu ya Buku,” Alisema Heaven.

Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage, alisema kwamba njia ya ushindi ni kucheza mara nyingi zaidi ambapo pindi mtu anaposhinda hupewa zawadi yake kwa haraka, ambapo mpaka sasa zaidi ya wateja 32000 wamepatikana na jumla ya Sh Milioni 80 zimelipwa kwa washindi nane tu.

“Mpaka sasa tumefanya droo kubwa za kuwania Sh Milioni 10 nane na tayari wateja wameshapewa stahiki zao hivyo kuifanya Biko kutoa Sh Milioni 80 kwa washindi wake nane ukiacha wale wanaolipwa papo kwa hapo ambao ndio wengi na wanatoka kila mikoa ya Tanzania,” Alisema.

Droo kubwa ya kuwania Sh Milioni 10 inayochezeshwa na Biko inafanyika mara mbili kwa wiki ambapo ni Jumatano na Jumapili, huku mshindi wa zawadi za papo kwa hapo akipatikana kila baada ya dakika chache.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...