https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, May 23, 2017

Muchunguzi: Kuogopa kucheza Biko ni dalili ya kukaribisha umasikini

Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage, kulia akimkabidhi nyaraka halali za Benki ya NMB zinazoonyesha kuingizwa kwa fedha za mshindi wao Sospeter Muchunguzi pichani kushoto jumla ya Sh Milioni 10 alizoshinda katika Bahati Nasibu yao ya Ijue Nguvu ya Buku, droo iliyochezeshwa Jumapili. Makabidhiano hayo yamefanyika jana jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MSHINDI wa droo ya saba ya Sh Milioni 10 kutoka kwenye Bahati Nasibu ya Biko 'Ijue Nguvu ya Buku', Sospeter Muchunguzi, amekabidhiwa fedha zake huku akisema kuwa kuogopa kucheza Biko ni dalili ya kukaribisha umasikini.



Muchunguzi aliyasema hayo jana katika benki ya NMB jijini Dar es Salaam wakati anakabidhiwa fedha zake na Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage.



Akizungumza kwa msisitizo mkubwa, Muchunguzi mwenye ndoto za ujasiriamali alisema kwamba watu wote waliofanikiwa katika maisha yao walithubutu katika mambo waliyokusudia kuyafanya, hivyo ni budi kila mmoja kupita njia hiyo.
Sospeter Muchunguzi katikati akisaini nyaraka za benki ya NMB kwa ajili ya fedha zake kuingizwa kwenye akaunti yake katika benki hiyo jana baada ya kuibuka kidedea katika droo ya Biko ya Sh Milioni 10. Kulia ni Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko Grace Kaijage na kushoto ni Afisa wa NMB.


Alisema uhakika wa kushinda ni mkubwa ikiwa mtu ameamua kweli kuingia katika sekta ya michezo ya kubahatisha, hususan mchezo wa Biko ambao hata uchezaji wake upo wazi na hakuna dalili zozote za kudanganya washindi.



“Nilipoona utaratibu wa Biko ni mzuri nikathubutu kucheza huku nikiamini kwamba endapo naweza kuibuka na ushindi naweza kusogea katika hatua moja kwenda nyingine hivyo Watanzania wenzangu hakuna haja ya kuogopa ili tusonge mbele.


“Nimefurahi kupata fedha hizi kutoka Biko maana hata uchezaji wao kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kufanya miamala kwenye simu za Tigo, Vodacom na Airtel kwa kuandika kuingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na kumbukumbu namba ya 2456 ni rahisi hali inayoweza kumfanya kila mtu amudu kucheza mahala popote na wakati wowote,” Alisema Muchunguzi.



Naye Grace Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, aliwataka Watanzania kila pembe za nchi kucheza kwa wingi ili wajiwekee mazingira ya kushinda zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja zinazotoka kila wakati, huku pia donge nono la Sh Milioni 10 likitolewa katika droo ya Jumatano na Jumapili.



“Lengo letu ni kutoa zawadi nono kwa kila mshindi wetu, hivyo umnachotakiwa kufanya ni kucheza Biko kwa wingi kwa kununua tiketi kuanzia Sh 1000 na kuendelea ili mshinde, maana kucheza mara nyingi zaidi ndio njia ya kufanikisha ushindi,” Alisema Grace na kuongeza kuwa tiketi moja inatoa nafasi mbili, ikiwamo ya ushindi wa papo kwa hapo pamoja na nafasi ya kuingia kwenye droo ya kuwania Sh Milioni 10.



Kwa mujibu wa Grace, washindi wao wanaoshinda zawadi za papo kwa hapo wanatumiwa fedha zao kwa kupitia simu walizocheza na wale wa droo kubwa wakikabidhiwa katika benki ili kuleta usalama wa fedha wanazotoa kwa washindi wao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...