https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, February 15, 2016

Bondia Said Mbelwa kuvaana na Ibrahim Tamba, Machi 26 Dar es Salaam

Promota Jaffari Kitemo 'katikati' akiwainua mikono juu mabondia Ibrahimu Tamba kushoto na Said Mbelwa wakati wa utambulisho wa mpambano wao jana utakaofanyika march 26 katika ukumbi wa frends corner Manzese, Dar es Salaam. 
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MABONDIA Ibrahimu Tamba na Said Mbelwa jana wamesaini mkataba wa kuzipiga march 26 katika ukumbi wa Frends corner manzese Dar es salaam, mpambano uho wa raund nane kg 76 umeratibiwa na  Jaffari Kitemo.

Akizungumza mara baada ya kutiliana saini mikataba ya kuzipiga Kitemo alisema kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mbalimbali ya utangulizi ukiondoa pambano hili na tumeandaa mpambano uhu kwa ajili ya kuondoa ubishi wa nani zaidi mana kila mmoja anatamba mtaani kuwa yeye ni zaidi ya mwenzie sasa jibu tutalipata Machi 26 pale Manzese

Naye bondia Mbelwa amesema kuwa kawaida yake ni kugawa dozi kwa kumpatia kipigo kitakatifu Tamba akijibu majigambo hayo Tamba amesema mkuwa yeye ana makuu huvyo atakikisha anafanya mazoezi ya kutosha kwa ajili ya kumpiga Mbelwa kwani ngumi ni ngumi tu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...